TUNAOMBA RADHI KWA PICHA::Majambazi wawili wauwawa na Jeshi la Polisi mkoani Geita ..Ni baada ya kufanya Uporaji. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Thursday, June 26, 2014

TUNAOMBA RADHI KWA PICHA::Majambazi wawili wauwawa na Jeshi la Polisi mkoani Geita ..Ni baada ya kufanya Uporaji.


Watu wawili wanaodhaniwa kuwa ni majambazi wakiwa na  bunduki moja aina ya SMG , yamemvamia mfanyabiashara wa maduka ya M-Pesa mkoani Geita na kumuua kwa kumpiga risasi kisha kumpora fedha.


Hata hivyo, majambazi wawili waliohusika katika tukio hilo waliuawa na polisi kwa kushirikiana na wananchi baada ya tukio hilo.

Majambazi yamemvamia mfanyabiashara wa maduka ya M-Pesa mkoani Geita na kumuua kwa kumpiga risasi kisha kumpora fedha.Hata hivyo, majambazi wawili waliohusika katika tukio hilo waliuawa na polisi kwa kushirikiana na wananchi baada ya tukio hilo.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Geita, Joseph Konyo, alithibitisha kutokea kwa mauaji hayo pamoja na mfanyabiashara huyo kuporwa kiasi cha fedha ambacho hata hivyo, hakijajulikana.

Kamanda Konyo alisema tukio hilo lilitokea juzi June 24,2014,jioni saa 11.30 jioni, katika kata ya Kalangalala mjini Geita.


Kamanda Konyo amemtaja mfanyabiashara aliyeuawa na majambazi hao kuwa ni Gosbert Walwa (54), ambaye alipigwa risasi kadhaa maeneo ya tumboni na kwamba alifariki dunia muda mfupi baada ya kufikishwa katika Hospitali ya Wilaya ya Geita kwa ajili ya matibabu.

Kamanda Konyo alisema majambazi hao walikuwa na bunduki moja aina ya SMG ambayo waliitumia katika uporaji na mauaji hayo.

Hata hivyo, majambazi wawili waliohusika katika tukio hilo waliuawa na polisi kwa kushirikiana na wananchi baada ya tukio hilo.


Pia majambazi hao walifanya uporaji kwa wakala mkuu wa bia mjini humo Bw.Ignas Athanas na kupora Sh. milioni 1.8 pamoja na bastola yenye namba HO478Y ikiwa na risasi 15 inayomilikiwa kihalali na mfanyabisahara huyo.



Kamanda huyo alisema kuwa wakati polisi wakielekea katika eneo la tukio, majambazi hayo tayari yalikuwa yameshatoroka kwa kutumia pikipiki aina ya SANLG yenye namba T460 CVQ hiyo.

Aidha majambazi hao waliokuwa na bunduki aina ya SMG iliyofutwa namba zake na risasi 13 na simu ya mkononi aina ya TECNO huku wakiwa wamevalia makoti meusi na helment ili kuficha sura zao zisitambulike kwa urahisi.

Jeshi la polisi lilipata taarifa muda mfupi zilizotolewa na raia wema ambapo kamanda wa polisi akiongoza kuwafatilia majambazi hao walifanikiwa kuwakuta katika pori lililopo jirani na kijiji cha Ibambila wilayani Nyangh’hwale zaidi ya km 50 kutoka mjini Geita walipofanya uharifu.

Wakiwa wanakimbizana majambazi hao walipowaona askari jambazi mmoja aliyekuwa na silaha aliruka kwenye pikipiki na kuanza  kuwashambulia askari kwa risasi lakini dereva wa polisi alimfuata moja kwa moja na kumgonga kwa gari jambazi huyo na kufariki hapo hapo.

 Baada ya hapo jambazi mwingine alikimbia kwa pikipiki na askari wakaanza kumfukuza wakishirikiana na wanafunzi wa shule ya sekondari Nyang’hwale na kufanikiwa kumkamata na kuanza kumshambulia na alifariki wakati anakimbizwa kupelekwa hospitali.

Taharuki hiyo iliyokuwa imeukumba Mji wa Geita kwa saa takribani 3 kabala hawajakamatwa majira ya saa 2 huku  baadhi ya wananchi wamelipongeza jeshi la polisi kwa kazi waliyoifanya kwa mda mfupi mara baada ya tukio hilo huku kamanda Konyo akiendelea kuwaasa wananchi wazidi kutoa ushirikiano kwa jeshi la polisi ili kuimarisha amani katika mkoa huo.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad