SAFU YA UONGOZI CUF:-Naibu Katibu Mkuu CUF Bara aliyechukua nafasi ya Julius Mtatiro anusurika katika ajali- Picha Ziko Hapa Jionee ..’ - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Monday, June 30, 2014

SAFU YA UONGOZI CUF:-Naibu Katibu Mkuu CUF Bara aliyechukua nafasi ya Julius Mtatiro anusurika katika ajali- Picha Ziko Hapa Jionee ..’


Naibu Katibu m kuu mpya wa CUF pia Mbunge wa viti Maalum Magdalena Sakaya akimshukuru Mungu baada ya kunusurika katika ajali na Lori kwenye makutano ya barabara ya Mandela na Nyerere Dar es Salaam.



Naibu Katibu m kuu mpya wa CUF pia Mbunge wa viti Maalum Magdalena Sakaya akimshukuru Mungu baada ya kunusurika katika ajali na Lori kwenye makutano ya barabara ya Mandela na Nyerere Dar es Salaam.Picha Na:-Robert Okanda.


HATIMAYE Chama cha Wananchi (CUF) kimekamilisha mchakato wa kuchagua safu ya uongozi wa Kitaifa kwa kuwachagua wajumbe 45 wa Baraza Kuu la Uongozi Taifa na 20 kati yao wakitokea Zanzibar.

Wajumbe hao ni miongoni mwa 143 waliogombea Baraza Kuu la Uongozi kupitia Kanda saba za Tanzania Bara na mbili za Zanzibar ambazo ni Kanda ya Unguja na Kanda ya Pemba.

Kuchaguliwa kwa wajumbe hao kumekamilisha safu ya Uongozi wa kitaifa ambapo Juni 25 mwaka huu, wajumbe wa mkutano mkuu walimchagua tena Prof. Ibrahim Lipumba kuwa Mwenyekiti na Maalim Seif Sharif Hamad kuendelea kuwa Katibu Mkuu.

Wajumbe hao pia walimchagua Juma Duni Haji kuwa Makamu Mwenyekiti akichukua nafasi ya Machano Khamis Ali ambaye hakugombea tena.

Akizungumza baada ya uchaguzi huo, Prof. Lipumba aliwashukuru wajumbe wa mkutano mkuu kwa kuonyesha nidhamu ya hali ya juu na kufanikisha uchaguzi huo kwa amani na usalama.

Alisema hatua hiyo imedhihirisha ukomavu wa demorasia na uvumilivu ndani ya chama hicho, na kuwataka wajumbe waliochaguliwa kuendeleza kazi ya kukiimarisha na kukijenga chama hicho, ili kiweze kushinda katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2015.

Waliochaguliwa

Wajumbe 10 wanaowakilisha Baraza Kuu Kanda ya Unguja ni Salim Bimani, Nassor Ahmed Mazrui, Fatma Abdulhabib Ferej, Zahra Ali Hamad na Shaaban Iddi Ahmed.

Wengine ni Pavu Juma Abdallah, Abdillahi Jihadi Hassan, Hassan Jani Massoud, Mohd Kombo Ali na Hemed Said Nassor.

Kanda ya Pemba, wajumbe 10 ni Hamad Massoud Hamad, Abubakar Khamis Bakar, Rukia Kassim, Said Ali Mbarouk na Khalifa Mohd Issa.

Wengine ni Omar Ali Shehe, Riziki Omar Juma, Massoud Abdallah Salim, Hijja Hassan Hijja na Najma Khalfan Juma.


Miongoni mwa wajumbe 25 wa Baraza Kuu la Uongozi Taifa kutoka Bara ni Chifu Letalosa Yemba, Lobora Petro, Fatma Omar Kalembo, Magdalena Sakaya, Thomas Malima na Kapasha wa Kapasha.

Wengine ni Bonifasia Mapunda, Abdul Juma Kambaya, Ashura Mustapha, Karume Jeremia, Julius Nyanja Salim Sarwan na Katani Ahmed Katani.




No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad