Ushindi 3-2 wa Simba SC waifanya ifikishe pointi 35 nyuma ya Mbeya City yenye pointi 36, Ligi Kuu Vodacom Tanzania bara. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Monday, March 03, 2014

Ushindi 3-2 wa Simba SC waifanya ifikishe pointi 35 nyuma ya Mbeya City yenye pointi 36, Ligi Kuu Vodacom Tanzania bara.

Jonas Mkude akimpongeza Tambwe baada ya kufunga  bao mbili na kufikisha sasa magoli  19 msimu huu wa Ligi Kuu Tanzania bara na moja la Haruna Chanongo zimewapa Simba ushindi wa Bao 3-2 dhidi ya Ruvu Shooting kwenye Mechi ya , Ligi Kuu Vodacom iliyochezwa Jana March 02,2014, Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

 Mshambuliaji wa Simba Amri Kiemba, akijaribu kufunga bao katika mchezo wa Ligi kuu Tanzania Bara uliochezwa kwenye Uwanja wa Taifa Dar es Salaam.
Kocha Mkuu wa Simba Logarusic, akiwaelekeza wachezaji wake kama ilivyokawaida yake ambapo katika mchezo huo Simba ilishinda Bao 3-2 dhidi ya Ruvu Shooting.
Mashabiki wa Simba wakishangilia moja ya bao la simba SC baada ya jana March 02,2014,kupata ushindi wa mabao 3-2 dhidi ya Ruvu Shooting katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Ushindi huo, unaifanya Simba SC ifikishe pointi 35 baada ya kucheza mechi 19 na kuendelea kubaki nafasi ya nne  nyuma ya Mbeya City yenye pointi 36, Yanga pointi 38 na Azam FC pointi 40 kileleni.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad