Picha ya Shekhe na Mtoto wamemwagiwa kimiminika kinachodhaniwa kuwa ni tindikali mkoani Arusha. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Saturday, March 01, 2014

Picha ya Shekhe na Mtoto wamemwagiwa kimiminika kinachodhaniwa kuwa ni tindikali mkoani Arusha.


Shekhe wa msikiti mkuu wa bondeni, Arusha, Mustapha Mohamed Kiago (49) akiwa yupokatika hospital ya mkoa Maunt Meru akipatiwa matibabu baada ya kumwagiwa tindikali yeye na mtoto wake picha ya chini na mtu asiyejulikana ambaye hawakumtambua.

Mtoto Halidi Mustapha Mohamed (10) akiwa amejeruhiwa baada ya kumwagiwa tindikali yeye pamoja na baba yake.

Sheikh wa Msikiti Mkuu wa Bondeni mkoani Arusha,Mustapha Mohamed Kiago na mwanaye Khalid Mustapha mwenye umri wa miaka 10, wamemwagiwa kimiminika kinachodhaniwa kuwa ni tindikali wakati wakiingia msikitini jana Februari 28,2014.

Sheikh  Kiago amejeruhiwa shingoni na mtoto wake ameumizwa machoni na wote wanatibiwa katika hospitali ya mkoa wa Arusha ya Mount Meru.

Sheikh Kiago amesema amemwagiwa tindikali hiyo jana majira ya saa 11.10 alfajiri wakati anashuka ngazi kuingia msikitini kuongoza sala ya alfajir.

Kwa upande wake Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Bw Japhet Lusingu, akizungumzia tukio hilo, amesema polisi ina taarifa za tukio hilo na kwamba inaendelea na uchunguzi.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad