CHEKI:-Matokeo ya Jumla ya Uchaguzi Mdogo wa Ubunge Jimbo la Kalenga-mkoani Iringa ,CCM ikiibuka na Kicheko. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Monday, March 17, 2014

CHEKI:-Matokeo ya Jumla ya Uchaguzi Mdogo wa Ubunge Jimbo la Kalenga-mkoani Iringa ,CCM ikiibuka na Kicheko.

Mgombea Ubunge Uchaguzi mdogo wa Jimbo la Kalenga, Iringa Vijijini, kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Bw.Godfrey Mgimwa  akiwa amebebwa na wafuasi wa chama hicho jana March 16,2014, usiku katika Ofisi ya CCM Mkoa wa Iringa baada kutangazwa matokeo ya awali yasiyo rasmi .Chama cha Mapinduzi (CCM) kimeibuka na ushindi wa kishindo kwa kushinda kata zote 13 zilizoko kwenye jimbo hilo la Kalenga. 



Matokeo ya Uchaguzi Mdogo jimbo la Kalenga - Iringa vijijini yametangazwa rasmi jana March 16,2014, usiku na Tume ya Taifa ya Uchaguzi mjini Iringa,kuwa chama cha Mapinduzi ( CCM)  kilipata jumla ya kura 22945,na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA),Kilipada idadi ya jumla kura 5800 na chama cha CHAUSTA kilipata kura 143.

Hivyo chama cha CCM kilishinda kwa asilia 79.4,CHADEMA asilimia 20.1 na CHAUSTA asilimia 0.5.Matokeo hayo ni ya jumla kwa Kata 13 za jimbo hilo.

Kwa mujibu wa Tume ya Uchaguzi, Watu 71, 765 walitarajiwa kupiga kura katika vituo 216, lakini  kwa Mujibu wa Waandishi wa Habari waliokuwa wakifuatilia uchaguzi huo mdogo wa Ubunge, walisema kulikuwa na idadi ndogo ya watu waliojitokeza katika baadhi ya vituo, huku wengi wakilalamika kushindwa kupiga kura kutokana na kupoteza vitambulisho vyao.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad