Kala Jeremiah aelezea matokeo mabaya ya kuibiwa page ya Facebook, ni baada ya wezi kuitumia ili kumgombanisha Diamond na Ali Kiba. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Thursday, February 27, 2014

Kala Jeremiah aelezea matokeo mabaya ya kuibiwa page ya Facebook, ni baada ya wezi kuitumia ili kumgombanisha Diamond na Ali Kiba.


Msanii anawewakilisha Jiji la Mwanza, Kala Jeremiah anazidi kupata hasara zaidi kufuatia kuibiwa kwa ukurasa wake wa facebook na ‘hackers’ waliamua kutumia jina lake kuingiza pesa kwa njia za udanganyifu, huku wakipost maelezo mengine ambayo yanawaacha mdomo wazi baadhi ya watu ambao bado wanaamini akaunti hiyo inamilikiwa na rapper huyo.

Jumatano (February 26,2014) ilizagaa habari kwenye mitandao ya kijamii iliyowekwa na wezi hao ‘hackers’, habari ambayo ililenga moja kwa moja katika kuwakosanisha wakali wa Bongo Flava Diamond Platinumz na Ali Kiba huku jina la Kala Jeremiah likitumika kuiuza zaidi habari hiyo kwa kuonekana kuwa yeye ndiye aliyeandika.

Kala ameongea na tovuti ya Times Fm na kuelezea jinsi ambavyo tukio hilo lilivyomsikitisha, na kudai kuwa ingawa hakuwasiliana na wasanii hao anaamini kabisa kuwa kupitia maelezo anayoyatoa kwenye media wameelewa kuwa sio yeye bali ni watu walioiteka akaunti yake ya Facebook.

Jana limezuka lingine la kupost mikopo sijui nini halafu wakawataja na wasanii na hiyo ndio mbaya zaidi kwa sababu wanawagombanisha wale wasanii, halafu wanawagombanisha wale wasanii kupitia mimi. 

Kwa hiyo kwa mtu mwingine ambaye hana uelewa zaidi, au ukikuta msanii mwenyewe akawa hana uelewa zaidi unaweza kujikuta na yeye anakumaindi, yaani kwa ujumla sio kitu kizuri.” Kala Jeremiah ameiambia tovuti ya Times Fm.

“Lakini hayo yote mimi namuachia Mungu kwa sababu Mungu ndiye anayenijua mimi kiundani. Hawa watu ni binadamu wanafanya hayo lakini ipo siku…kwa sababu wote tuko chini ya jua, hawawezi kujua mimi nilihustle kiasi gani kuifikisha hiyo page hapo halafu mtu anaitumia kufanya anavyotaka yeye, anaitumia anavyotaka yeye, anaandika vitu anavyotaka yeye.” Ameongeza.

Amewataka watanzania kufahamu kuwa ile page ya Facebook yenye ‘likes’ zaidi ya 50,000 kwa sasa sio yake tena na kwamba kuna wahuni ambao wanaitumia.

Katika ukurasa huo wa facebook aliopokonywa Kala mwaka jana, wezi hao wameanza kuwatapeli watu kwa kuonesha kuwa Kala Jeremiah anatangaza kutoa mikopo kwa riba nafuu.

Katika hatua nyingine, rapper huyo yuko katika hatua za mwisho za kushuti video ya Remix ya wimbo wake Wale Wale, aliyofanya na Juma Nature, Young Killer na Ney Lee.

Usikose kusikiliza The Jump Off ya 100.5 Times Fm kwa undani wa habari hii, na utamsikia Kala Jeremia akifafanua kwa undani jinsi alivyopata hasara kufuatia kuibiwa kwa ukurasa wake wa Facebook.

Sorce:-Times.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad