 |
|
Abiria
arobaini na nane waliokuwa wakisafiri na basi la shabiby kutoka Mkoani Arusha
kuelekea Mkoani Dodoma wamenusurika kufa huku 28 wakijeruhiwa baada ya basi lao
kutaka kulipita lori la mafuta wakati basi lingine la Princes Munaa nalo likiwa
linalipita basi la Shabiby katika mlima Kisaki na kusababisha basi la
Shabiby kuanguka.
|
 |
| Wakieleza
kondakta wa basi hilo aina ya Yunton lenye usajili wa namba T 930 BUW ambaye
amevunjika miguu yote miwili bwana Thadei Muhando na mkaguzi wa basi la
Shabubu bwana Williamu Ofyenge wamesema wakati basi lao lilikuwa liki lipita lori
la mafuta gafla waliona basi lingine liki wapita na kuwa magari matatu
katika njia moja na hatimaye dereva wao alishindwa kulimudu basi lao na
kusababisha kupinduka. |
 |
| Kwa upande
wake dereva wa roli la mafuta aina ya benzi lenye usajili wa namba raa 496n na
tela lake lenye usajili wa namba rl 0255 ambalo lilikuwa likitokea nchi
ya Rwanda bwana Hadimana Benjamini amesema alipitwa na mabasi mawili na
moja likamgonga upande wake na hatimaye kuanguka . |
Mganga
mfawidhi wa Hospitali ya Mkoa wa Singida Daktali Banuba Deogratius
amethibitisha kupokea majeruhi ishirini na nane ambao wanapatiwa matibabu
na mgonjwa moja ambaye alikuwa kondakta wa basi amevunjika miguu yote miwili na
wanampatia matibabu.
Mkuu wa
wilaya ya Singida Mwl.Queen Mlozi ambaye alifika katika ajali hiyo pamoja
na kuwatembelea majeruhi amewataka madereva wote kuzingatia sheria za
barabarani ilikuweza kunusuru uhai wa watu na majeruhi.
No comments:
Post a Comment