Mahakama kuu
nchini Rwanda imemuhukumu kiongozi wa upinzani nchini humo Bi .Victoire
Ingabire kutumikia kifungo cha miaka 15 gerezani baada ya kumkuta na hatia ya
uhaini.
Hukumu hiyo
imetolewa baada ya Bi Ingabire kukata rufaa akipinga adhabu iliyotolewa awali
ya kutumikia kifungo cha miaka 8 gerezani.
Mahakama
imemtia hatiani Bi Ingabire kwa makosa ya ugaidi, kuchochea chuki miongoni mwa
raia wa Rwanda na kuhusika na mauaji ya halaiki dhidi ya nchi hiyo mwaka 199.
Awali mwezi
Oktoba, Bi Ingabire ambaye ni wa asili ya ki Hutu alipatikana na hatia ya
ugaidi, na kukana kutokea mauaji ya kimbari dhidi ya kabila la wa Tutsi.
Mauaji hayo
yalifanyika mwaka wa 94 ambapo zaidi ya watu 800 wa kabila la wa Tutsi
waliuawa.
Bi Ingabire
alikata rufaa dhidi ya hukumu ya awali aliyopewa ya kifungo cha maisha jela
baada ya kukutwa na makosa ya uhaini kwa kufadhili makundi ya kigaidi na kuhusika
katika mauaji ya halaiki ya mwaka 1994 japo upande wa mashtaka nao ulitaka
aongezewe hukumu hiyo na hata kupendekeza apewe hukumu ya maisha gerezani.
Shirika la
kutetea haki za binadamu la Amnesty International limeshutumu namna kesi ya Bi
Ingabire imeendeshwa.
Bi Ingabire
amekumbwa na matatizo na sheria ya Rwanda baada ya kurejea nchini humo
mwaka 2009, kutoka Uholanzi alikoishi
kwa miaka kadhaa.
Alieleza
wazi nia yake kuwania urais nchini humo lakini hakupata fursa kwani punde tu
alipowasili alifunguliwa mashtaka hayo.
Kutokana na
kujivuta kwa kesi yake, hakushiriki uchaguzi uliofuata wa mwaka wa 2010. Tangu
wakati huo, amekuwa kizuizini.
Amekuwa
akiwakilishwa na wakili kutoka Uingereza ambapo 2010 ambapo ameendelea
kusisitiza kuwa hajafanya makosa yaliyoelekezwa kwake na kwamba hukumu hiyo ina
msukumo wa kisiasa.
No comments:
Post a Comment