Tazama Taswira ya msongamano wa malori kwenye kituo cha Forodha cha Rusumo wilayani Ngara mkoani Kagera huku Serikali ya Rwanda ikishusha ushuru kwa wiki moja. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Wednesday, September 04, 2013

Tazama Taswira ya msongamano wa malori kwenye kituo cha Forodha cha Rusumo wilayani Ngara mkoani Kagera huku Serikali ya Rwanda ikishusha ushuru kwa wiki moja.

Madereva wanaotumia Mpaka Rusumo wilayani Ngara mkoani Kagera kusafirisha Bidhaa kwenda nchi za Rwanda na DRC wanasema  kupanda kwa tozo la ushuru kutoka  dola 152 za Kimarekani hadi dola 500  kumewaathiri Kisafari na hata ilielezwa kwamba Maafisa wa forodha wa kituo cha Rusumo katika mkoa wa Kibungo nchini Rwanda kushindwa kutoa huduma kwa madereva hao wanaotokea Tanzania.

Magari hayo yamekaa kwa muda wa siku nne tangu Septemba Mosi,Mwaka huu baada ya nchi ya Rwanda kuongeza kiwango cha ushuru  kutoka Dola za Marekani 152 (Sh240,000) kuwa Dola 500 (Sh790,000) .






Afisa Mfawidhi wa kituo cha Forodha  cha Rusumo wilayani Ngara mkoani Kagera Bw.Nassoro Ibrahim anasema kuwa Septemba Mosi,Mwaka huu,Magari katika kituo hicho yalikuwa 63 ambapo Hadi Jana(Septemba 3,2013) Magari  yalifikia 194 na kufanya Jumla kwa siku tatu  Kufikia  magari 332.




Akizungumza na waandishi wa habari mjini Dodoma jana(Septemba 03,2013), Naibu Waziri wa Uchukuzi, Dk Charles Tizeba alisema ushuru unaotumika ni ule wa zamani badala ya mpya na kwamba alishauriana na Waziri wa Miundombinu wa Rwanda, Profesa Silas Rwakabamba na kukubaliana ushuru wa zamani utumike wakati Serikali hizo zikiendelea na mashauriano. 



Ni Taswira ya msongamano wa malori kwenye kituo cha Forodha  cha Rusumo wilayani Ngara mkoani Kagera huku  Serikali ya Rwanda ikishusha ushuru kwa wiki moja.



Kutokana na hali hiyo Kamera yetu iliwashuhudia Madereva  wakipata usumbufu wa gharama za maisha ikiwa ni pamoja na kutafuta jinsi ya kujipikia kwa kukosa fedha za kununua chakula hotelini na wengine kukutwa uvunguni mwa magari  yao wakipika chakula ili  kujikimu na njaa huku  bei za vitu kwa wafanya biashara wa Rusumo ikipandishwa-mfano sahani ya chakula badala ya Tsh.2000 sasa ni Tsh.3500 hadi Tsh.4000 na kwa madereva wasiokuwa na fedha za safari wanabaki kuombaomba ama kusaidiwa na wenzao.







Balozi wa Rwanda nchini Tanzania ,Bw.Ben Rugangazi anasema Sasa tumeamua kuchukua hatua hii ili kwenda sambamba na wenzetu Tanzania na pande zote Tanzania na Rwanda zilikubaliana kuwa ushuru mpya ungeanza kutumika Septemba mwaka huu.
Kitendo cha nchi ya Rwanda kupandisha ushuru wa magari yatokayo Tanzania kuingia nchini humo na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo(DRC) baadhi ya madereva wa kitanzani watokao bandari ya Dar es Salaam kusafishisha mizigo kwenda katika mchi hizo wamekwama kwa siku nne kwenye kituo cha forodha cha Rusumo wilaya ya Ngara mkoani Kagera.

Mmoja wa madereva hao  Ally Rashid Masoud anayefanya Kazi katika kampuni ya Halgan Transport  ya Jijini Dares Salaam amesema kuwa tangu Septemba Mosi,Mwaka huu  wamekaa mpakani  hapo na mizigo ndani ya  magari bila kupata ufumbuzi wa tatizo hilo.

Masoudi amesema kuwa wanaoendesha magari ya mizigo kutoka bandari ya Dar es Salamu kuelekea katika nchi za Rwanda na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo  kupitia mpaka wa Rusumo wamekwama kwa siku nne katika kituo cha Forodha  cha Rusumo wilayani Ngara mkoani Kagera baada ya kupandishiwa ushuru wa magari kuingia nchini Rwanda.

Kwa upande wake Afisa Mfawidhi wa kituo cha Forodha  cha Rusumo wilayani Ngara mkoani Kagera bw.Nassoro Ibrahim amesema tangu tozo hiyo ianze msululu wa magari kukaa katika kituo hicho umekuwa mkubwa  ukilinganisha na awali kabla ya ongezeko la ushuru huo.

Bw.Nassoro Ibrahim anasema kuwa Septemba Mosi,Mwaka huu,Magari katika kituo hicho yalikuwa 63 ambapo Hadi Jana(Septemba 3,2013) Magari  yalifikia 194 na kufanya Jumla kwa siku tatu  Kufikia  magari 332.

Hata hivyo amesema kuwa kwa sasa serikali mbili kati ya Tanzania na Rwanda wako kwenye mazungumzo ya kusitisha zoezi hilo la kupanda kwa ushuru ili kujenga mahusiano na kukuza uchumi wa kibiashara bila kuleta madhara kwenye jamii za nchi hizo.

Wakati huo huo, Balozi wa Rwanda nchini Tanzania ,Bw.Ben Rugangazi alisema kuongezwa kwa ushuru huo wa forodha kisichukuliwe kama jaribio la kutaka kuvuruga uhusiano kati ya nchi hizi mbili.

Balozi Rugangazi alisema Rwanda imeamua kupandisha kiwango chake kutoka Dola za Marekani 152 (Sh240,000) kuwa Dola 500 (Sh790,000) ambazo pia hutozwa na Serikali ya Tanzania kwa muda mrefu.

Amesema Kumekuwa na majadiliano ya muda mrefu ili kuleta ulinganifu wa ushuru wa forodha kwani kwa muda mrefu wafanyabiashara Rwanda wamekuwa wakilalamika kutokana na kushindwa kushindana vizuri kwenye soko la biashara kutokana na tofauti kubwa ya ushuru wa forodha.

Balozi Rugangazi anasema Sasa tumeamua kuchukua hatua hii ili kwenda sambamba na wenzetu Tanzania na pande zote Tanzania na Rwanda zilikubaliana kuwa ushuru mpya ungeanza kutumika Septemba mwaka huu.

Aidha Kutokana na msongamano wa malori kwenye mpaka wa nchi hizo mbili, Serikali ya Rwanda imeshusha ushuru kwa wiki moja.

Akizungumza na waandishi wa habari mjini Dodoma jana(Septemba 03,2013), Naibu Waziri wa Uchukuzi, Dk Charles Tizeba alisema ushuru unaotumika ni ule wa zamani badala ya mpya.

Tizeba alisema alishauriana na Waziri wa Miundombinu wa Rwanda, Profesa Silas Rwakabamba na kukubaliana ushuru wa zamani utumike wakati Serikali hizo zikiendelea na mashauriano.

Alisema Mawaziri wa Fedha wa Tanzania na Rwanda walitazamiwa kukutana ili kuzungumzia suala hilo.

Dk Tizeba alisema  wafanyabiashara wa Tanzania walipata usumbufu mkubwa baada ya kulazimika kulipa Dola 500 kuingiza mizigo yao Rwanda badala ya Dola 152.


Hata hivyo, alikanusha madai kuwa Rwanda imepandisha ada hizo kutokana na mgogoro wa kisiasa baina ya nchi hizo.

Habari/Picha Na:Mwanawamakonda na Shaaban Ndyamukama.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad