Mkuu
wa Mkoa wa Kagera Kanali mstaafu Fabian Masawe kushoto akiwa na Wakuu wa Mikoa
kutoka Nchini Burundi nyuma yao ni Mkuu
wa wilaya ya Ngara mkoani Kagera nchini Tanzania Bw.Kostantine Kanyasu.
|
Wajumbe
wa kamati ya ardhi kutoka Tanzania na Burundi wakibadilishana mawazo njeya
kikao chao wilayani Ngara mkoani Kagera.
|
Mkuu
wa Mkoa wa Kagera Bw.Fabian Masawe akifafanua jambo kwa mwandishi wa habari
Bw.Shaaban Ndyamukama.
|
Wataalamu
wa masuala ya mipaka ya kimataifa kutoka Burundi wakiwa nje ya Ukumbi wa
Halmashauri ya Ngara baada ya kikao na
wenzao wa Tanzania.
|
Viongozi
wandamizi kutoka nchini Burundi na Tanzania
wamekutana katika wilaya ya Ngara mkoani
Kagera kwenye mkutano wa sita wa ujirani mwema kujadili changamoto za kimipaka
baina ya nchi hizo kwa wananchi wanaoingiliana kimataifa katika shughuli za uzalishaji mali.
Mkuu
wa mkoa wa kagera kanali mstaafu Fabiani Masawe akifungua mkutano huo leo(September 02,2013) amewataka wataalamu wa mipaka ya kimataifa
kutoka mataifa hayo kufanya kila linalowezekana kuinyoosha mipaka ya nchi hizo
jirani na kuondoa migogoro kwa wananchi walioko katika nchi hizo.
Kanali
Masawe amesema kuwa migogoro ya kuhamisha alama za kimataifa zinazotenganisha
taifa moja na jingine imeanza kuibuka mwaka 1983 na mataifa hayo kuwa na mikutano
ya mazungumzo bila kupata suluhisho kwa
wananchi wake .
Amesema
wakulima na mataifa ya Tanzania na Burundi walioko mipakani wanalazimika
kuanzisha uhasama na kuvunja mahusiano yao kwa kugombania mahali pa kulima na
kulishia mifugo na migogoro hiyo kuwa mikubwa kasha kuingizwa kwenye vikao vya
kimataifa .
“Mipaka hii imekuwa ya kurithi kutoka kwa wakoloni
ambayo iliwekwa bila kushirikisha watu wa maeneo husika na waaasisi wa mataifa
haya wameongoza bila migogoro lakini ilikuwa ni kutokana na uchache wa
watu kwenye mataifa yao”.Alisema Masawe.
Aidha
alidai kuwa wataalamu wa nchi hizo hawana budi kukubaliana na kuweka alama
ambazo kwa namna moja au nyingine imeondolewa na mabadiliko ya hali ya hewa
kama mito na vijito ama kwa kukauka au kufurika na kuhama njia za awali.
Alisema
kuna haja ya kutekeleza maazimio ya pamoja kwa vitendo katika nchi jirani ili kuweka alama ambazo hazitafutika au
kuondolewa na watu wenye nia ya kuingilia taifa jingine ambazo ni za kisasa
katika mfumo wa digitali na si kuendelea na mfumo wa analojia ambao umepitwa na
enzi.
Katika
hatua nyingine Kanali Masawe alisema kuwa mikutano ya kubaini mipaka kupitia Umoja
wa Afrika ilikuwa itekelezeke hadi 2012kisha kushindwa na sasa muda umeongezwa hadi 2017 hivyo mataifa hayo yatumie muda huo kupanga
bajeti ya kuwezesha maazimio ya AU yaweze kufanikiwa.
Awali
katika kikao hicho mkuu wa wilaya ya
Ngara Costantine Kanyasu alisema kuwa migogoro ya kimipaka kati ya Tanzania na
Burundi japo sio kubwa lakini wakazi wa kijiji cha Kasange Mugoma na Mukikomero
wanaingiliana kwa shughuli za kilimo na kanza kuhitilafiana wakati wa mavuno.
Bw.Kanyasu
alidai kuwa vigingi vya kimipaka vilivyopo maeneo hayo baadhi yake vimeng’olewa
na wahalifu wanaodhani katika kusimikwa kwake kuna madini yalichimbiwa ardhini
ma kuvifukua na kupasua kuona kilichomo ndani ya vigingi hivyo.
Alifafanua
kuwa pamoja na wananchi wa wilaya hiyo na mikoa ya Muyinga pamoja na Chankuzo nchini Burundi kuwa na mahusiano mema
kuna haja ya alama za kimataifa kati ya taifa na jingine kutambulika kwa
wananchi hao na kuishi kwa usalama na amani.
Hata
hivyo Wakuu wa mikoa ya Muyinga ,Chankuzo Ruyigi na Makamba wamedai Tanzania haina mahusiano mabaya na Nchi ya Burundi na changanoto mbalimbali za kimahusiano ukiwemo ulinzi na
usalama zitamalizwa kwa njia za
vikao ili kulinda amani kwa watu wa
mataifa hayo.
Kiongozi
wa wakuu hao Nilagira Berikimas alisema mikutano na vikao vya mara kwa mara kwa
kushirikisha wataalamu wa fani mbalimbali zikiwemo kamati za ulinzi na usalama
za nchi hizo hakutakuwa tena na mtafaruku wa kimazingira kuhusu mahusiano yao.
“Sote
tuko ndani ya Afrika na Jumuia ya afrika
ya Mashariki hivyo la msingi nikuitana kuja Tanzania au Burundi na kufanya
mazungumzo na maazimio ya pamoja kuyatekeleza kuanzia ngazi za vitongoji” .Alisema Berikimas.
Aliongeza
kuwa siku za hivi karibuni miezi miwili iliyopita kulikuwa na vikao vya pamoja
baina ya viongozi wa wilaya ya Ngara na mikoa ya Muyinga na Chankuzo kujadili
mahusiano katika usalama na jinsi ya kukuza biashara kwa wananchi kuuziana
na kubadilishana bidhaa.
Wajumbe
kutoka Tanzania katika mkutano huo walikuwa
ni wataalamu wa mipaka ya kimataifa kutoka wizara ya ardhi, wizara ya Nishati na
Madini, wizara ya maji na mazingira, ofisi ya waziri mkuu na ofisi ya Rais pamoja
na ofisi ya waziri wa mambo ya nje na
ushirikiano wa kimataifa.
Picha/
Habari Na: Shaaban Ndyamukama
No comments:
Post a Comment