MABINGWA
watetezi wa Ligi Kuu Vodacom, Yanga SC Jana(Agosti 24,2013) wameanza kampeni yao ya kutetea Taji
lao huko Uwanja wa Taifa Jijini Dar es Salaam kwa kuitwanga Timu iliyopanda
Daraja Msimu huu, Ashanti United, Mabao 5-1.
Bao
za Yanga SC zilifungwa na Jerry Tegete, Bao 2, Msuva, Niyonzima na Nizar Khalfan
wakati lile la Ashanti lilifungwa na Shaban Juma alieingizwa Kipindi cha Pili.
Kikosi cha Jana(Agosti 24,2013) cha Coastal Union, hiki kilichoanza dhidi ya Oljoro JKT na waliichapa JKT Oljoro Bao 2-0 kwa Bao za Abdi Banda. |
![]() |
Wachezaji
wa Timu za Mbeya City na Kagera Sukar wakisalimia kabla ya kuanza mchezo wao
katika Uwanja wa Sokoine ambapo timu hizo zilitoka sare ya bila kufungana.
|
Huko
Manungu, Mtibwa Sugar na Azam FC zilitoka Sare Bao 1-1 huku Mtibwa wakitangulia
kufunga katika Dakika ya 4 kwa Bao la Luizio na Azam FC kusawazisha katika
Dakika ya 33 kwa Bao la Penati ya Aggrey Morris.
Nao
Coastal Union, wakicheza Ugenini huko Arusha, waliichapa JKT Oljoro Bao 2-0 kwa
Bao za Abdi Banda, Dakika ya 10, na Bao jingine la Dakika ya 29 ni la kujifunga
wenyewe JKT Oljoro.
Toka
Tabora, Timu mpya Rhino Rangers ilitoka Sare ya Bao 2-2 na Simba SC huku Bao zote
mbili za Simba SC zikifungwa kwa Penati za Jonas Mkude na Bao za Rhino kufungwa na
Noel na Kipanga.
LIGI
KUU VODACOM 2013/2014.
Jumamosi
Agosti 24,2013.
Yanga
5 Ashanti 1
Mtibwa
Sugar 1 Azam FC 1
JKT
Oljoro 0 Coastal Union 2
Mgambo
JKT JKT Ruvu
Mbeya
City 0 Kagera Sugar 0
Ruvu
Shooting 3 Prisons 0
Rhino
Rangers 2 Simba 2
RATIBA
YA LIGI KUU VODACOM:
Jumatano
Agosti 28,2013.
Mtibwa
Sugar v Kagera Sugar
Rhino
Rangers v Azam FC
JKT
Ruvu v Prisons
Mbeya
City v Ruvu Shootings
Mgambo
JKT v Ashanti United
JKT
Oljoro v Simba
Yanga
v Coastal Union
SERIE
A -ITALIA 2013/2014.
![]() |
AC Milan |
Ligi kuu ya SERIE A huko Italia ilianza Jana (Agosti 24,2013) kwa Luca Toni,
Mkongwe wa Miaka 36, kuipigia Timu yake iliyopanda Daraja Hellas Verona Bao 2
na kuibwaga AC Milan 2-1 na Mchezaji mpya Carlos Tevez kufunga Bao pekee wakati
Mabingwa Juventus walipoifunga Sampdoria Bao 1-0 Ugenini.
AC
Milan walitangulia kwa Bao la Dakika ya 14 alilofunga Andrea Poli ambae alikuwa
akiichezea Klabu yake mpya Mechi ya kwanza tu.
Lakini
vichwa viwili vya Mkongwe Luca Toni, Mchezaji wa zamani wa Kimataifa wa Italy,
vya Dakika za 29 na 53 viliipa Hellas Verona ushindi wa Bao 2-1 katika Mechi
yao ya kwanza ya Msimu mpya wa Ligi na pia ikiwa ni mara yao ya kwanza kucheza
Serie A katika Miaka 11.
Ushindi
huo ulileta furaha kubwa na hoihoi kwa Mashabiki wa Hellas Verona waliojazana
Stadio Bentigodi ambao kwa Miaka mingi waliteseka wakiona Timu yao ikigaagaa
Madaraja ya chini ya Ligi yale ya Pili na ya Tatu wakati Mahasimu wao wakubwa
wa Mji mmoja, Chievo Verona, wakimeremeta Ligi kubwa ya Serie A.
![]() |
Juventus
striker Carlos Tevez has admitted he had enjoyed the "perfect night"
after scoring on his debut in the 1-0 win over Sampdoria in front of his former
Manchester City boss Roberto Mancini.
|
Huko Mjini Genoa, Bao pekee la Mechi kati ya Wenyeji Sampdoria na Mabingwa Juventus
lililofungwa na Carlos Tevez katika Mechi yake ya kwanza kabisa ya Serie A
liliipa ushindi Juventus wa Bao 1-0.
Bao
hilo llifungwa katika Dakika ya 58 kufuatia kazi nzuri ya Arturo Vidal na Paul
Pogba kwenye Kiungo.
Katika
Dakika ya mwisho, Sampdoria walibaki Mtu 10 wakati Paolo Castellini,
alieingizwa toka Benchi, kumchezea rafu mbaya Stephan Lichtsteiner na kupewa
Kadi Nyekundu.
Serie
A inaendelea tena leo(Agosti 25,2013) kwa Mechi 7 na kesho Jumatatu Usiku iko Mechi moja.
SERIE
A 2013/2014 RATIBA/MATOKEO.
Jumamosi
Agosti 24,2013.
Hellas
Verona 2 AC Milan 1
Sampdoria
0 Juventus 1
Jumapili
Agosti 25,2013.
[Saa
za Bongo]
19:00
Inter Milan v Genoa
21:45
SS Lazio v Udinese
21:45
Parma v Chievo Verona
21:45
Torino FC v Sassuolo
21:45
Napoli v Bologna
21:45
Livorno v AS Roma
21:45
Cagliari v Atalanta
Jumatatu
Agosti 26,2013.
21:45
Fiorentina v Catania
LIGI
KUU ENGLAND 2013/2014.
![]() |
Daniel Sturridge |
Liverpool
Jana(Agosti 25,2013) wameendeleza ushindi wao wa pili katika Mechi zao mbili za
kwanza za Ligi Kuu England kwa Msimu huu mpya wa 2013/14 baada ya Straika wao
Daniel Sturridge kufunga Bao pekee Uwanjani Villa Park na kuwatungua Wenyeji
Aston Villa Bao 1-0.
Katika
Mechi ya kwanza ya Ligi Jumamosi iliyopita, Liverpool waliifunga Fulham Bao 1-0
na Mfungaji alikuwa Daniel Sturridge.
Bao
hilo la Sturridge lilifungwa katika Dakika ya 21 na hilo ni Bao lake la 8
katika Mechi 7 za Ligi alizocheza kuanzia Msimu uliopita.
Mara
ya mwisho kwa Liverpool kushinda Mechi zao mbili za kwanza za Msimu mpya ni ule
Msimu wa 2008/09.
Ligi
Kuu England inaendelea Jumapili kwa Mechi mbili kati ya Cardiff City na
Manchester City na nyingine n kati ya Tottenham na Swansea City.
LIGI
KUU ENGLAND MATOKEO.
Jumamosi
24 Agosti,2013.
Fulham
1 Arsenal 3
Everton
0 West Bromwich Albion 0
Hull
City 1 Norwich City 0
Newcastle
United 0 West Ham United 0
Southampton
1 Sunderland 1
Stoke
City 2 Crystal Palace 1
Aston
Villa 0 Liverpool 1
Jumapili
25 Agosti,2013.
18:00
Cardiff City v Manchester City
18:00
Tottenham Hotspur v Swansea City
Jumatatu
26 Agosti,2013.
22:00
Manchester United v Chelsea
BUNDESLIGA UJERUMANI 2013/2014.
MABINGWA
wa Ujerumani , Bayern Munich, Jioni ya jana(Agosti 24,2013) wamepata ushindi wao wa tatu mfululizo
kwenye Msimu mpya wa Ligi ya Bundesliga walipoifunga 2-0 Nuremberg Uwanjani
Allianz Arena na wao kuwa moja ya Timu 4 ambazo zimeshinda Mechi zao zote za
Ligi hiyo tangu ianze.
Timu
nyingine ambazo zimeshinda Mechi zote 3 ni Borussia Dortmund, Bayer Leverkusen
na Mainz.
Katika
Mechi yao ya jana , Bayern Munich walikosa Penati katika Kipindi cha Kwanza
iliyopigwa na David Alaba na Kipa wa Nuremberg Raphael Schaefer kuokoa lakini
Kipindi cha Pili walifunga Bao zao zote mbili.
Bao
la kwanza la Bayern lilifungwa na Franck Ribery kwa kichwa cha Dakika ya 69 na
kisha Arjen Robben akapachika Bao la pili katika Dakika ya 78.
![]() |
Bayern Munich boss Pep Guardiola paid tribute
to match-winners Franck Ribery and Arjen Robben after the pair scored in the
2-0 win over Nurnberg on Saturday.
|
Katika
Mechi hii Bayern walishusha Kikosi kikali kilichokamilika hasa kwenye Kiungo
ambapo Mawinga walikuwa ni Robben na Ribbery na katikati walikuwa Viungo
Wachezeshaji Thiago Alcantara na Mario Gotze.
Jumanne
Bayern watacheza Mechi ya Ligi na Freiburg na Ijumaa wataruka kwenda Monaco
kucheza Mechi ya UEFA Super Cup dhidi ya Chelsea.
BUNDESLIGA
RATIBA/MATOKEO:
Ijumaa
Agosti 23,2013.
Borrussia
Dortmund 1 Werder Bremen 0
Jumamosi
Agosti 24,2013.
Bayern
Munich 2 Nurnberg 1
Hannover
2 Schalke 1
Hoffenheim
3 Freiburg 3
Leverkusen
4 Monchengladbach 2
Mainz
2 Wolfsburg 0
Hertha
1 Hamburg 0
Jumapili
Agosti 25,2013.
16:30 Eintracht Braunschweig v Eintracht
18:30 Augsburg v Stuttgart
No comments:
Post a Comment