Takribani
watu 37 wameripotiwa kupoteza maisha Mjini Kuala Lumpur nchini Malaysia ,baada ya basi
walilopanda kutumbukia katika korongo refu.
Maafisa wa
usalama nchini humo wamesema ajali hii ni moja ya ajali kubwa ambazo zimewahi
kutokea, kutokana na kusababisha vifo vya watu wengi.
Baadhi ya
abiria wameokolewa kutoka katika korongo hilo ambalo lina urefu wa futi 200
hali iliyosababisha waokoaji kutumia cranes pamoja na kamba kuweza kuokoa
majeruhi wa ajali hiyo.
Ripoti zinasema kwamba basi hilo lilibeba abiria
wapatao 49 na mpaka sasa ni abiria 16
waliokolewa wakiwa hai japokuwa hali zao bado ni mbaya na huenda idadi
ya vifo ikaongezeka.
Licha ya
kutokea ajali iyo maafisa wa usalama wameshindwa kutambua uraia wa wahanga wa
ajali iyo.
![]() |
Baadhi ya
abiria wameokolewa kutoka katika korongo hilo ambalo lina urefu wa futi 200
hali iliyosababisha waokoaji kutumia cranes pamoja na kamba kuweza kuokoa
majeruhi wa ajali hiyo.
|
No comments:
Post a Comment