![]() |
Rais wa
Zimbabwe Comrade Robert Gabriel Mugabe amekula kiapo cha kuitumikia nchi hiyo
kwa muhula wa 7 mfululizo katika sherehe zilizofanyika mjini Harare, August 22,
2013.
|
![]() |
Rais Robert
Mugabe wa Zimbabwe ashika bibilia akila kiapo wakati wa sherehe za kuapishwa
kwake mjini Harare na ameahidi
"kuilinda na kuitetea katiba ya Zimbabwe".
|
![]() |
Rais Robert
Mugabe na mkewe Grace waikiwapungia mkono umati wa watu alipokuwa anawasili
kwenye uwanja wa michezo kuhudhuria sherehe za kuapishwa kwake mjini Harare,
August 22, 2013.
|
![]() |
A supporter
of Zimbabwean President Robert Mugabe attends his inauguration in Harare,
August 22, 2013.
|
![]() |
Mfuasi wa rais
Robert Mugabe akibeba bango la rais wakati wa sherehe za kuapishwa kwake mjini
Harare, August 22, 2013.
|
Rais wa Zimbabwe Comrade Robert Gabriel Mugabe amekula kiapo cha kuitumikia nchi hiyo kwa muhula wa 7 mfululizo katika sherehe zilizofanyika mjini Harare.
Katika kiapo mbele ya Jaji Mkuu Godfrey Chidyausiku maelfu ya wafuasi
wake, Mugabe ameahidi "kuilinda na kuitetea katiba ya Zimbabwe".
Wakuu wa nchi 40 walikuwa wamealikwa katika sherehe hizo, ambazo zimesusiwa
na upinzani.
Msemaji wa kiongozi wa upinzani nchini humo, Morgan Tsvangirai, alisema
kiongozi huyo hawezi kushiriki katika kile alichokiita 'sherehe ya mwizi'.
Tofauti na sherehe zilizopita kumwapisha Mugabe ambazo hazikuwa na
shamrashamra, hii ya mwaka huu imepewa umuhimu mkubwa ambapo Maelfu ya raia
wapatao elfu 60 walihudhuria sherehe hizo ambazo pia viongozi mbalimbali wa
bara la Afrika walialikwa.
Sherehe hizo
zimefanyika baada ya mahakama kutupilia mbali kesi iliyowasilishwa na upinzani
kupinga matokeo hayo na kumtangaza rais Mugabe kama mshindi halali huku pia
viongozi wa MDC wakiwa hawajaalikwa kwenye sherehe hizo.
Ma rais
kadhaa wa bara la Afrika tayari wamewasili jijini Harare kuhudhuria katika
sherehe hizo.
Hivi majuzi
viongozi wa Jumuiya ya kiuchumi ya nchi za kusini mwa Afrika SADC waliitaka jamii
ya kimataifa kuiondolea vikwazo Zimbabwe, baada ya uchaguzi kufanyika katika
hali tulivu.
Marekani
tayari imetangaza kuindolea vikwazo Zimbabwe pale tu rasi mugabe atakuwa tayari
kufanya mageuzi kwa mujibu wa matakwa ya wananchi wake.
Rais Mugabe
anatimiza mwaka wa 33 madarakani na kuwa mmoja kati ya viongozi wa Bara la
Afrika aliyekaa madarakani kwa muda mrefu zaidi huku mwenyewe akitamba kutaka
kuongoza taifa hilo mpaka atakapofikisha umri wa miaka 100.
Hivi sasa
rais Mugabe ana umri wa miaka 89 na ameapishwa
kwa ajili ya muhula mwengine wa miaka mitano kuliongoza taifa hilo la Zimbabwe na
wachambuzi wanaonya kuwa amri ya mahakama hiyo kutupilia mbali madai ya
Tsvangirai aliyepinga matokeo ya uchaguzi ni kichocheo cha ukandamizaji wa
kisiasa.
Tume ya
Uchaguzi nchini Zimbabwe ilitangaza kuwa chama cha ZANU-PF kilishinda theluthi
tatu ya idadi ya viti bungeni na kwamba Mugabe alipata ushindi wa zaidi ya
asilimia 60 ya kura zilizopigwa.
Lakini wiki
iliyopita Tsavangirai alifutilia mbali madai yake dhidi ya ZANU-PF, baada ya
kuyapeleka katika Mahakama Kuu kupinga matokeo ya uchaguzi, akisema hana imani
ya kupata haki mahakamani huko. Siku ya Jumanne mahakama hiyo ilisema uchaguzi
huo ulikuwa huru na haki na kuwa ulizingatia matakwa ya raia wake.
Tsvangirai
anadai kuwa takribani wapiga kura milioni moja waliondolewa kwenye vituo vya
kupigia kura katika maeneo ya mijini yanayoaminiwa kuwa ni ngome yake ya
kisiasa, ingawa mahakama ilifutilia mbali madai hayo.
Hata hivyo,
msemaji wa Tsvangirai, Douglas Mwonzora, ameiambia IPS kuwa hakushangazwa na
uamuzi uliotolewa na mahakama hiyo, kwa kuwa walilijua suala hilo mapema.
Sherehe za
kuapishwa kwa Rais Mugabe zilikuwa zimecheleweshwa kufanyika kutokana na kesi
hiyo.
Source:DW.
Source:DW.
No comments:
Post a Comment