|
Hii
ndiyo hali halisi ya Mji mdogo wa Tunduma leo April 02,2013 kuanzia asubuhi, Matairi yanachomwa katikati ya barabara.(Picha
na Mbeya yetu .
|
|
Hii
ndiyo hali halisi ya Mji mdogo wa Tunduma leo April 02,2013 kuanzia asubuhi, Matairi yanachomwa katikati ya barabara.
|
Diwani
wa kata ya Tunduma Ndugu Frank Mwaijoka (Chadema) pamoja na mchungaji wa kanisa
la KKT katika eneo hilo la Tunduma wilayani Momba Mkoani Mbeya wametakiwa
kujisalimisha kituo cha Polisi Tunduma mara baada ya kuhusika na uchochezi wa
kidini hali ambayo imepelekea kutokea kwa vurugu katika eneo hilo.
Vurugu
hizo zimeanza majira ya saa 3:asubuhi katika eneo hilo la Tunduma mara baada ya
kundi la watu wanaodai kuwa wao ni wafuasi wa dini ya kikristo wakidai
waruhusiwe kuchinja mifugo na kuuza katika mabucha yao hali iliyo pelekea
kuibuka kwa vurugu hizo.
Akizungumza
kuhusiana na tukio hilko Kamanda wa Polisi Mkoani humo Ndugu Diwani Athumani
amesema kuwa kufuatia kuwepo kwa tukio hilo jumla ya watu zaidi ya 40 tayari
wamekwisha kamatwa .
Amesema
mpaka sasa taarifa walizo zipata kufuatia vurugu hizo zinaeleza kuwa miongoni
mwa watu walichochea vurugu hizo ni diwani wa kata hiyo ya Tunduma Ndugu John
mwaijoka pamoja na Mchungaji wa kanisa la kkt ndugu Neema Mwaipusa ambao kwa
pamoja wametakiwa kujisalimisha kituo cha polisi kwa mahojiano zaidi.
Amesema
suala hilo limegubikwa na siasa kwani tayari viongozi wa serikali akiwemo
Mkuu wa mkoa huo Ndugu Abbas Kandoro amekwisha litolea ufafanuzi Apri 02 mwaka
huu wakiwepo pia viongozi wa dini .
Amesema
kwa asilimia kubwa mgogoro huo juu ya nani achinje umeingiliwa na mambo ya
kisiasa kwani hata baadhi ya wananchi wa maeneo hayo wamekuwa wakilalamika juu
ya kutokea kwa vurugu hizo.
Amesema
shughuli za kibiashara katika eneo hilo zimeshindwa kufanyika katika eneo hilo
hivyo kufanya wananchi kupata adha hasa kwa nchi jirani ya Zambia ambao kwa
asilimia kubwa wanategema kupata mahitaji kutoka mpakani mwa Tanzania.
Hata
hivyo Diwani amesema kuwa katika vurugu hizo askari mmoja pamoja na mwananchi wamejeruhiwa kwa kupigwa
mawe ambapo tayari wamekwisha fikishwa kituo cha polisi.
Kufuati
hali hiyo Kamanda huyo wa Polisi amesema kwa sasa hali imelejea katika hali yake
ya kawaida hivyo amewataka wananchi wa maeneo hayo kuwa watulivu wakati jeshi
hiulo la Polisi likiendela na msako wa kuwatafuta wahalifu wengine.
![]() |
|
Mambo
hayo .
|
Picha
na Mbeya yetu .






No comments:
Post a Comment