Manchester United sasa wawa Pointi 15 mbele dhidi ya Mabingwa watetezi Manchester City baada kuichapa QPR na Ryan Giggs kupachika Bao la pili katika Mechi yake ya 999 kwa Klabu na Nchi yake. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Sunday, February 24, 2013

Manchester United sasa wawa Pointi 15 mbele dhidi ya Mabingwa watetezi Manchester City baada kuichapa QPR na Ryan Giggs kupachika Bao la pili katika Mechi yake ya 999 kwa Klabu na Nchi yake.



Man United
Manchester United leo wakicheza ugenini Uwanja wa Loftus Road wameifunga Timu ya mkiani QPR Bao 2-0 na kufungua pengo la Pointi 15 mbele ya Mabingwa watetezi Man City walio nafasi 3 ambao kesho Jumapili wanaivaa Chelsea ambao wako nafasi ya 3 Pointi 19 nyuma ya Man United.




Bao la kwanza la Man United lilifungwa katika Dakika ya 23 na Rafael kwa kigongo kikali nje ya boksi kilichomshinda Mbrazil mwenzake Kipa Cesar.



Bao la Giggs lilifungwa katika Dakika ya 80 baada ya ushirikiano mwema na wenzake na Danny Welbeck kumpenyezea pande tamu na kumalizia.



Katika Dakika ya 41 Staa wa Man United, Robin van Persie, alilazimika kutolewa baada kujikwaa na Kamera pembeni mwa Uwanja na nafasi yake kuchukuliwa na Wellbeck.





MATOKEO



Jumamosi Februari 23




Cazorla Dakika ya 6 & 85
Fulham 1 Stoke City 0

Arsenal 2 Aston Villa 1

Norwich City 2 Everton 1

Queens Park Rangers 0 Manchester United 2

Reading 0 Wigan Athletic 3

West Bromwich Albion 2 Sunderland 1




Jumapili Februari 24




[Saa 10 na Nusu Jioni]



Manchester City v Chelsea

Newcastle United v Southampton



Jumatatu Februari 25

[Saa 5 Usiku]

West Ham United v Tottenham Hotspur


No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad