 |
| Wema Abrahamu Sepetu |
Msanii wa
tasnia ya filamu Bongo, Wema Abrahamu Sepetu kutangaza kuwa anamiliki kampuni
mpya ya filamu"Endless Fame Film" leo mchana aliweza kufanya press
conference na waandishi mbalimbali huku akitambulisha rasmi kampuni hiyo.
Wema
anasema Kwa mujibu wa msanii huyu
alisema kwamba kwa sasa bado ofisi yake
haijaanza kufanya kazi ila inatarajia rasmi kuanza kazi mwezi wa tatu mwaka
huu.
Tazama picha za ofisi yake mpya 'Endless
Fame Film' iliyoitambulisha leo rasmi.......
 |
Japokua
mwigizaji Wema Sepetu hakua tayari kutaja kiasi cha pesa kilichogharimu ofisi
yake mpya aliyoifungua, amekubali kwamba ilimchukua miezi 6 toka ameanza
kuishughulikia, ni ofisi ambayo itahusika kwa kiasi kikubwa kuandaa movie zake
pamoja na movie za waigizaji wengine.
Mpaka sasa
ameshatoa ajira kwa vijana wenzake sita na bado anasema kuna nafasi za ajira
kwa vijana ambao wanadhani wanavigezo vya kufanya kazi ya utengenezaji movie
wakiwa ni wataalamu wa vitu mbalimbali.
Kampuni hiyo
itakua pia inahusika na kuvifanyia kazi vipaji vya waigizaji wapya na kuwapa
nafasi ya kuonekana wakiwa tayari na mikataba mizuri chini ya usimamizi wa Wema
Sepetu likiwa pia ni moja ya malengo yake kwenye hiyo kampuni.
Mama mzazi
wa Wema anasema anamshukuru sana Marehemu Kanumba manake ndio alimshawishi ampe
Wema ruhusa ya kuingia kwenye uigizaji mpaka kutimiza ndoto kama hii.
|
 |
Wema na Dotnata
|
 |
Mama mzazi
wa Wema katika ofisi ya Wema ambayo ipo ghorofa ya kwanza kwenye nyumba ambayo
ipo Kinondoni Dar es salaam karibu na Biashara Complex.
|
 |
Wema na
Zamaradi
|
 |
Wema na Rich
|
No comments:
Post a Comment