![]() |
| Sulley Muntari |
FC Barcelona wakiwa na Mchezaji Bora Duniani, Lionel Messi, wameonja joto katika mchezo wa soka ndani ya uwanja wa San Siro huko Jijini Milano Italia, baada ya kubondwa Bao 2-0 na wenyeji wao AC Milan katika Mechi ya kwanza ya Raundi ya Mtoano ya Timu 16 ya UEFA CHAMPIONS LIGI.
Frikiki ya AC Milan ilipenyezwa kwa Riccardo Montolivo alieachia kigongo kilichobabatiza Wachezaji kadhaa na kutua kwa Kevin-Prince Boateng aliefunga Bao la kwanza kwa AC Milan katika Dakika ya 57.
Bao la pili lilifungwa na Sulley Muntari katika Dakika ya 81 baada ya kazi nzuri ya M'Baye Niang na Stephan El Shaarawy.
Huko Uturuki kwenye nyingine , Galasaray,
wakiwa na wapya Didier Drogba na Wesley Sneijder, walikamatwa na kutoka sare ya
Bao 1-1 na Schalke ya Ujerumani.RAUNDI YA MTOANO YA TIMU 16 RATIBA.
[Mechi zote kuanza Saa 4 Dak 45 Usiku]
MARUDIANO
Jumanne 5 Machi 2013
Borussia Dortmund v Shakhtar Donetsk [2-2]
Man United v Real Madrid [1-1]
Jumatano 6 Machi 2013
Juventus v Celtic [3-0]
Paris St Germain v Valencia [2-1]
Jumanne 12 Machi 2013
![]() |
| Bayern Munich v Arsenal |
Schalke v Galatasaray [1-1]
Jumatano 13 Machi 2013
Bayern Munich v Arsenal [3-1]
Malaga v FC Porto [1-0]
ROBO FAINALI.
Mechi ya 1=Tarehe 2 na 3 Aprili 2013
Mechi ya 2= Tarehe 9 na 10 Aprili 2013
NUSU FAINALI.
Mechi ya 1= Tarehe 23 na 24 Aprili 2013
Mechi ya 2= Tarehe 30 Aprili na 1 Mei 2013
FAINALI
25 Mei 2013
UWANJA wa WEMBLEY, London.







No comments:
Post a Comment