Cheki Nyama inayotajwa kuwa ni chanzo cha Vurugu kubwa za kidini kati ya Waislamu na Wakristo katika kijiji cha Buseresere huku Mtu mmoja akifariki na watu 10 wakijeruhiwa vibaya kwa mapanga . - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Tuesday, February 12, 2013

Cheki Nyama inayotajwa kuwa ni chanzo cha Vurugu kubwa za kidini kati ya Waislamu na Wakristo katika kijiji cha Buseresere huku Mtu mmoja akifariki na watu 10 wakijeruhiwa vibaya kwa mapanga .



Picha:Nyamba ambayo inadaiwa Wakiristo  walikuwa wamechinja ng’ombe mmoja na mbuzi wawili eneo la kanisani kabla ya kuipeleka nyama hiyo katika bucha hiyo iliyoko eneo la Buseresere Sokoni na ndipo walipokumbana na kadhia.



Katika Vurugu  hizo  kubwa za kidini kati ya Waislamu na Wakristo, zimezuka katika kijiji cha Buseresere, wilaya ya Chato, mkoani Geita, na kusababisha kifo cha Mchungaji wa Kanisa la Pentekoste Assemblies of God, Mathayo Kachila (45), huku watu wengine 10 wakijeruhiwa vibaya kwa mapanga.



Waraka unaotajwa kuwahamasisha wakristu kushiriki katika uzinduzi wa uchinjaji.

FFU kazini katika eneo la Buseresere  wilaya ya Chato, mkoani Geita katika hatua za kurejesha Amani na Utulivu.


Mkuu wa Wilaya ya Chato,Bw. Ludorick Mpogolo, aliyefika eneo la tukio muda mfupi baada ya polisi kuwasili, mbali na kusikitishwa na kitendo hicho aliwataka wananchi kuwa watulivu wakati serikali ikiangalia njia sahihi za kutatua mgogoro huo ambao unakua kwa kasi kila kukicha.


Hivi karibuni mgogoro huo wa kidini umezidi kukua wilayani humo kwa pande hizo mbili kila upande ukidai ndiyo wenye haki ya kuchinja nyama inayouzwa buchani.

Majeruhi Ramadan aliyejeruiwa wakati wa vurugu za waislam na wakristu wachache zilizotokea leo katika kijiji cha Buseresere wilayani Chato mkoani Geita na kusababisha fukuto kubwa la vurugu zilizosababisha shughuli mbalimbali kusimama.-


Picha Na: biharamulonews.blogspot.com

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad