Halmashauri ya wilaya Ngara mkoani Kagera yazuia mifugo kuingia wala kutoka katika wilaya hiyo kutokana na kuwepo kwa ugonjwa wa miguu na midomo. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Wednesday, February 13, 2013

Halmashauri ya wilaya Ngara mkoani Kagera yazuia mifugo kuingia wala kutoka katika wilaya hiyo kutokana na kuwepo kwa ugonjwa wa miguu na midomo.

mwanawamakonda.blogspot.com
Mifugo ya Ng'ombe.
Halmashauri ya wilaya Ngara mkoani Kagera imezuia mifugo kuingia wala kutoka katika wilaya hiyo kutokana na kuwepo kwa ugonjwa wa miguu na midomo.

 

Mganga wa mifugo wa wilaya ya Ngara Dr Richard Ngowi amesema hayo kupitia taarifa yake kwa vyombo ya habari na kwamba Karantini hiyo itaendelea hadi hapo idara yake itakapojiridhisha kumalizika kwa ugonjwa huo.




Amesema kuwa hairuhusiwi kusafirisha mifugo kutokana na maeneo mbalimbali ya wilaya ya Ngara kukabiliwa na ugonjwa wa miguu na midomo ili kukabilina na kuenea zaidi kwa ugonjwa huo.




Katika hatua nyingine Halmashauri ya wilaya ya Ngara imeufunga mnada wa mifugo wa Lumasi ulioko kata ya Kasulo kutokana na ugonjwa huo na kwamba watakaokiuka agizo hilo watachukuliwa hatua kali za kisheria.



Habari Na:Radio Kwizera FM

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad