Tanzania
imefanikiwa kushinda kupitia vivutio vyake vitatu vya utalii ambavyo ni Mlima
Kilimanjaro, Ngorongoro Crates na Mbuga ya wanyama ya Serengeti, hafla hiyo imehudhuriwa
na wageni waalikwa mbalimbali ikiwa ni pamoja na Mabalozi,Wafanya
biashara,Mawaziri, Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano ya Tanzania na wadau
mbalimbali wa utalii kutoka Mataifa mbalimbali katika ukanda wa Afrika
Mashariki.
Maajabu
mengine ni Red Sea, Mto Nile ambao zawadi yake ilichukuliwa na Uganda kama
asili ya mto huo na Jangwa la Sahara.
Bw Philip Imler Mwanzilishi wa Taasisi ya Seven Natural Wonders- alitaja wanyama saba wa ajabu Afrika,
ambao wote wako Tanzania akiwemo Chui, Tembo, Mamba, Kifaru, Kiboko, Sokwe Mtu
na Simba.
|
No comments:
Post a Comment