![]() |
Manchester City |
Katika mchezo Mwingine: Newcastle
walitoka nyuma kwa Bao 1-0 na kuishinda Southampton, iliyo nafasi za hatari za
kushushwa Daraja, Bao 4-2 katika Mechi iliyochezwa St James Park.
Ushindi huu umeipandisha Newcastle nafasi kadhaa katika
Msimamo wa Ligi Kuu England na sasa wapo nafasi ya 4 wakiwa na Pointi 30 zikiwa
ni Pointi ni Pointi 6 juu ya zile Timu 3 za mkiani ambayo ni sehemu ya hatari
kwani ni eneo la kuporomoka Daraja mwishoni mwa Msimu.
MSIMAMO.
1 . Manchester United Pointi
68
2 . Manchester City Pointi
56
3 . Chelsea Pointi 49
4 . Tottenham Pointi 48
5 . Arsenal Pointi 47
6 . Everton Pointi 42
7 . WBA Pointi 37
9 . Liverpool Pointi 39
![]() |
Real Madrid |
Huko
nchini Hispania katika La Liga: FC Barcelona walizidi kujiimarisha na kuwa na nafasi nzuri ya
kutwaa Ubingwa baada ya kuichapa Sevilla kwa Bao 2-1 hii
ikiwa ni Mechi yao ya kwanza toka wapokee kichapo kule San Siri mikononi mwa AC Milan katika mashindano ya
UEFA .
Sevilla
ndio waliotangulia kufunga kwa Bao la Botid
Dakika ya 42, na Barca
kusawazisha Dakika ya 51, kwa Bao la David Villa, na Lionel Messi kufunga Bao
la pili, Dakika ya 60.
Nao
Mabingwa watetezi Real Madrid na ushindi
wa bao 2 za kipindi cha Pili ,kupitia kwa Wachezaji wao
Gonzalo Higuain na Kaka, zimewapa ushindi wa
ugenini dhidi ya Deportivo La Coruna.
Deportivo
ndio waliotangulia kufunga kwa Bao la Dakika ya 34 la Riki na Real kupiga Bao
Dakika ya 73, Mfungaji Kaka, na Dakika ya 88 la Higuain.
Katika
mchezo huo Winga wa Real Angelo Di Maria alitolewa kwa Kadi Nyekundu Dakika ya 90
kufuatia Kadi za Njano mbili mfululizo.
MSIMAMO
1
Barcelona Pointi 68
2
Atletico Madrid Pointi 53
3
Real Madrid Pointi 52
4
Malaga Pointi 42
5
Valencia Pointi 41
6
Real Sociedad Pointi 40
![]() |
Borussia Dortmund |
Kwenye
Ligi ya Ujerumani : Bundesliga
Vinara Bayern Munich waliifumua Werder Bremen Bao 6-1 na kujichimbia kileleni wakiwa Pointi 18 mbele ya Mabingwa Borussia Dortmund ambao leo (Feb 24,2013 )wanacheza ugenini na Borussia
Mönchengladbach.
MSIMAMO
1 . Bayern Munich Pointi 60
2 .
Borussia Dortmund Pointi 42
3 .
Bayer Leverkusen Pointi 41
4 .
Eintracht Frankfurt Pointi 38
5 .
Freiburg Pointi 35
6 .
Hamburger Pointi 34
7 .
Hannover Pointi 33
8 .
Mainz Pointi 32
![]() |
AC Milan |
Aidha
AC Milan Jumapili hii wana
kibarua kipya kwenye Serie A watakapocheza Dabi ya Jiji la Milano na Mahasimu
wao wakubwa Inter Milan katika uwanja wa
San Siro, Uwanja ambao kwa Mahasimu hao
wote wawili ndio Nyumbani, huku AC Milan wakikamata nafasi ya 3 wakiwa na
Pointi 44 na Inter wapo nafasi ya 5 wakiwa na Pointi 43.
MSIMAMO
1
Juventus Pointi 55
2
Napoli Pointi 51
3
AC Milan Pointi 44
4
Lazio Pointi 44
5
Inter Milan Pointi 43
6
Fiorentina Pointi 42
7
Catania Pointi 39
No comments:
Post a Comment