Zambia |
Mechi hiyo ambayo ilitabiriwa kuwa moja ya mechi ngumu zaidi katika hatua ya
makundi ya fainali za kombe la mataifa ya Afrika inayoendelea nchini Afrika Kusini lakini ilianza kwa mashambukizi katika pande zote na
kunako dakika ya 25,mlinda lango wa Zambia Davies Nkausu alimfanyia madhambi
mshambulizi wa Nigeria Ahmed Musa na hivyo refa wa mechi hiyo kutoa penalti kwa
Nigeria.
Lakini mcheza kiungo wake John Obi Mikel ambaye pia anaichezea klabu ya Chelsea
akapoteza penalti hiyo na hivyo kuwapa Mabingwa hao watetezi nafasi nyingine ya
kupumua.
Katika kipindi hicho cha kwanza timu hizo mbili
zilionekana kutoshana nguvu huku pande zote zikifanya mashambulio ya mara kwa
mara.
Nigeria ilianza kipindi cha pili kwa kasi zaidi na
kufanya mashambulio kadhaa katika lango la Chipolopolo.
Na baada ya kupoteza mkwaju wa penalti John Obi
Mikel, alijiimarisha zaidi kipindi cha pili na kunako dakika ya 56 Nigeria
ikapata bao lake la kwanza kupitia kwa mshambulizi wake matata Emmanuel
Emenike.
Kunako dakika ya 84 mlinda lango wa Nigeria
alimuangusha mshambuliaji wa Zambia Emmanuel Mayuko, na refa wa mechi hiyo sawa
na alivyokuwa amefanya katika kipindi cha kwanza akaipa Zambia penalti ambayo
iliwekwa kimyani na kipa za Chipolopolo Kennedy Mweene.
Nigeria sasa ina alama mbili sawa na Nigeria na
itabidi washinde mechi zao za mwisho siku ya jumapili ili kufuzuz kwa hatua ra
robo fainal.
Awali Rais wa Nigeria Goodluck Jonathan, amewaandikia
wachezaji wa Super Eagles na kuwapa ushauri wa jinsi ya kucheza mechi hiyo.
Kocha wa Nigeria, Stephen Keshi, vile vile alifika
mbele ya viongozi wa shirikisho la mchezo wa soka nchini Nigeria, kuelezea kwa
nini hawakushinda mechi yao ya ufunguzi.
Mechi ya pili katika kundi hilo kati ya Ethiopia na
Burkina Faso kuanza mwendo wa saa tatu za usiku majira ya Afrika mashariki.
No comments:
Post a Comment