![]() |
Pamoja na
kwamba kulikuwa na Mvua kubwa lakini hakuna alitaka kuondoka msibani hapo mpaka
pale mwili ulipoondoka kuelekea Msikitini kwa Kusalia na baadae kwenye Mazishi.
|
Rais Jakaya
Mrisho Kikwete akiweka udongo katika kaburi la marehemu Sadick Juma Kilowoko
'Sajuki'.
|
Baba mzazi
wa Sajuki, Mzee Kilowoko, akiweka udongo katika kaburi la mwanaye.
|
![]() |
Makabulini
Kisutu Dar.
|
![]() |
Umati wa
watu uliojitokeza hapa katika makaburi ya kisutu upanga kumpumzisha mpendwa
wetu Sajuki.
|
Marehemu Sajuki’’alilazwa katika hospitali ya Muhimbili kwa wiki mbili ambapo alikua anasubiri kupata urahisi wa kusafiri kurudi India kwenye matibabu ambayo alipangiwa kurudi tena December 2012.
Mwezi wa
tano mwaka jana watanzania tulichanga kadri ya uwezo wetu ili akatibiwe
India.Ni kweli alienda India kwenye matibabu na alifanyiwa upasuaji.Ila
matibabu yake yalikuwa yakiendelea ambapo ilikuwa lazima arudi tena India mwezi
uliopita 2012.
Baada ya kurudi nchini hali yake ilikuwa nzuri
tu na mwili ukaanza kurejea kama anavyoonekana kwenye picha hapo akiwa na
Wastara mkewe.Pamoja na kuwa katika hali hii bado alikuwa ni mgojwa.

Mwezi wa
kumi na moja 2012 Sajuki alifanya tour aliyoiita asante Tanzania kwa lengo la
kuwashukuru watanzania walipomchangia.
Lakini kilichokuwa nyuma ya pazia ni
kwamba alikuwa akikusanya pesa ili arudi India kwa matibabu.
Akiwa mkoani Arusha katika Uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini hivi karibuni alianguka.Na yeye mwenyewe
kukiri kwa kusema “Sijisikii
vizuri, hali yangu ni mbaya.”
Baadae
mwenyewe alisema kuwa pamoja na kuumwa,haikuwa rahisi kurudi katika vyombo vya
habari tena kwa ajili ya kuomba Watanzania kumchangia kwa ajili ya fedha za
matibabu kwa awamu nyingine. na muda wa kurudi ulikuwa umefika.
Pamoja na
msaada lakini bado kulikuwa na changamoto kwamba tatizo kubwa lililomzuia
Sajuki kurudi India ni pumzi ambapo walikua wanatafuta ndege yenye huduma ya gesi.
Baada ya
kuhangaika sana, dakika za mwisho ndio walikua wamepata ndege ambayo imekubali
kutoa huduma ya gesi kwa Sajuki ambapo Shirika la ndege la Emirates ndio
lilikua limekubali kutoa huduma hiyo kumsafirisha mpaka India.
Sajuki
alikua na tatizo kubwa la kupumua wakati huu ambapo upumuaji wake ulikua unabadilika mara kwa
mara.
Pole sana Wastara ulijitahidi kadri ya uwezo
wako kuhakikisha mumeo anapona.
Ila yule aliyetuumba ndio ameamua na akipanga
lake hakuwa wa kulipangua.Pole kwa familia,mashabiki na watanzania kwa ujumla.
Kwa mujibu
wa baba yake mzazi,marehemu alizaliwa mwaka 1986 na amefariki akiwa na umri wa
miaka 27.
…. Mungu ailaze roho ya marehemu Juma Kilowoko (Sajuki) mahala pema peponi, Amen.
Inalillah waina_ilaih raahiun
ReplyDeletepumzika salama Sajuki, nilikupenda na kukubali na ntaendelea hivyo daima. R.I. P
ReplyDelete