Haruna
Chanongo aliyeruka
kufunga bao la kwanza la Simba SC
|
Katika
mchezo huo mabao ya Simba yalifungwa na kinda Haruna Athumani Chanongo
aliyepiga mawili, Felix Sunzu na Shomari Kapombe wakitupia kambani goli moja
kila mmoja.
Jamhuri ndio
walikuwa wa kwanza kuliona goli la Simba katika robo ya kwanza ya mchezo kwa
goli lilofungwa na Mfanyeje Mussa, kabla ya Simba kusawazisha katika dakika ya
27, na baadae kidogo akaongeza bao la pili kwa shuti kali,Mfanyeje tena
aliwaumiza tena Simba na timu zikaenda mapumziko zikiwa zimetoshana nguvu.
Awamu ya
pili ya mchezo Simba walirudi vizuri na kupata mabao mawili yaliyofungwa na
Felix Sunzu na Shomari Kapombe na kuipa timu yao ushindi wa kwanza ndani ya
mwaka 2013.
Aman Ibrahim Makungu. |
Kabla ya
mchezo huo, Makamu wa kwanza wa rais wa Zanzibar, Seif Sharrif Hamad alizindua
mashindano hayo kwa kupiga penalti na kumfunga kipa wa Jamhuri, Jaffar.
Akiongozwa na raisi wa Chama cha Soka Zanzibar
(ZFA), Aman Ibrahim Makungu, Mh Seif ambaye pia ni Katibu Mkuu wa CUF,
alizikagua timu zote mbili kabla ya kuanza kucheza.
Liewig
kushoto akisaini mkataba wa
miezi 18
kuifundisha Simba.
Kulia Makamu Mwenyekiti
wa Simba SC,
Geoffrey Nyange 'Kaburu'
|
Kocha mpya
wa Simba, Mfaransa Patrick Liewig alikuwa jukwaani akiishuhudia timu,
ikiongozwa na watakaokuwa wasaidizi wake, Mganda Moses Basena na mzalendo,
Jamhuri Kihwelo.
Katika
mchezo uliotangulia, Tusker ya Kenya iliichapa Bandari ya hapa mabao 5-1, mabao
ya Jesse Were 29 na 43, Ismail Dunga 35 Michael Olunga dakika ya 89 na Andrew
Tolowa dakika ya 90, wakati la Bandari lilifungwa na Amour Janja dakika ya
83.
No comments:
Post a Comment