Askari Polisi wawili wa kituo kidogo cha Polisi Kasulo wilayani Ngara mkoani Kagera wauwawa na Wananachi wa kijiji cha Chanyamisa wakidhaniwa kuwa ni majambazi. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Monday, January 07, 2013

Askari Polisi wawili wa kituo kidogo cha Polisi Kasulo wilayani Ngara mkoani Kagera wauwawa na Wananachi wa kijiji cha Chanyamisa wakidhaniwa kuwa ni majambazi.



IGP Said Mwema.

Askari Polisi wawili wa kituo kidogo cha Polisi Kasulo wilayani Ngara Mkoani Kagera wameuawa jana(Januari 6,2013) na wananachi wa kijiji cha Chanyamisa wilayani Karagwe mkoani humo wakidhaniwa kuwa ni majambazi.


 

Mkuu wa wilaya ya Ngara Bw Constantine Kanyasu amewataja waliouawa katika tukio hilo kuwa ni Sajent Thomas na Koplo Damas wote wa kituo cha Polisi Kasulo wilayani Ngara.



Bw Kanyasu amesema kuwa tukio hilo limetokea Januari 6 mwaka huu kati ya saa moja hadi saa nne usiku ambapo Askari hao wameuawa na wananchi baada ya kuanza kurusha risasi hewani waliposimamishwa na wananchi baada ya kuwekewa vizuizi barabarani wakidhaniwa kuwa majambazi.



Aidha amesema kuwa Askari hao ambao walikuwa wakitumia gari binafsi la askari mmoja wao wakiwa wamevaa kiraia ,baada ya kufika eneo hilo walishambuliwa na wananchi hadi kupoteza maisha na kwamba Askari aliyekuwa na silaha alifanikiwa kukimbia.



Bw Kanyasu amesema kuwa askari hao wa kituo cha Kasulo wilayani Ngara walikuwa na mtuhumiwa waliyemkamata akiwa na meno ya tembo lakini hawakutoa taarifa kwa uongozi wa wilaya ya Karagwe licha ya kupita katika vizuizi vya pori la Burigi mkoani Kagera.




Karagwe
Miili ya Askari Polisi  hao waliouwawa  imehifadhiwa katika hospitali ya Nyakahanga wilayani Karagwe.



Katika tukio hilo kijana mmoja aliyefahamika kwa jina la Juvenari Joseph amepigwa risasi kwenye kiganja na kulazwa katika hospitali ya Kayanga.



Kamanda wa polisi mkoani Kagera Bw Philip Kalangi amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kwamba uchunguzi unaendelea ili kubaini chanzo chake.

1 comment:

  1. Duh nyumbani Huko, Poleni wafiwa Na Asante kwa manewz ya ukweli Makonda

    ReplyDelete

Post Bottom Ad