![]() |
Uganda |
Wachezaji wa
Uganda wakimpongeza Geoffrey Kizito (anayetazama kamera amekumbatiana na
Kiiza), baada ya kufunga bao kwanza dakika ya nne dhidi ya Ethiopia katika Robo
Fainali ya Kombe la Mataifa ya Afrika Mashariki na Kati, CECAFA Tusker
Challenge kwenye Uwanja wa Mandela, Namboole mjini Kampala.
Uganda ilishinda
2-0 bao lingine likifungwa na Robert Ssentongo dakika ya 60 na kwa ushindi huo,
Uganda itamenyana na Tanzania Bara katika Nusu Fainali Alhamisi usiku, mchezo
ambao utatanguliwa na Nusu Fainali nyingine kati ya Kenya na Zanzibar.
![]() |
Kiiza,
Walusimbi, Wasswa wakicheza na Ssentongo.
|
![]() |
Harambee Stars |
Katika Robo Fainali ya
kwanza ya Kombe hilo la Mataifa ya Afrika Mashariki na Kati, CECAFA Tusker Challenge
Uwanja wa Mandela, Namboole, mjini Kampala, Uganda,Timu ya Kenya(Harambee Starz) ilishinda 1-0 dhidi ya Malawi, bao
pekee la Mike Barasa dakika ya 56 na sasa Harambee Stars itamenyana na Zanzibar
katika Nusu Fainali keshokutwa.
Wachezaji wa
timu ya Kenya na Malawi wakiwania mpiara wakati wa mchezo wa nusu fainali ya
mchezo wa Cecafa Challenge 2012 uliochezwa katika Uwanja wa Nelson Mandela
uliopo Nambole nchini Uganda
|
![](http://1.bp.blogspot.com/-wriaqirk0JE/ULJ-ZnRTWgI/AAAAAAAAK8k/A8GhUCKpwkA/s320/CECAFA_TUSKER_CUP_2012.jpg)
Akithibitisha
kuyeyuka kwa wenzao, Kocha wa Eritrea, Teklit Negash, amesema: “Hatujui Ndugu
zetu wako wapi!”
![]() |
Wachezaji
wa timu ya taifa ya Eritrea,
wana
sifa kubwa ya kutorokea nchi za watu,
kiasi
cha serikali ya nchi yao kuwawekea
sheria nguvu ya kuweka fedha za kwao
100,000
kama bondi kabla ya kusafiri.
|
Eritrea
ilitolewa kwenye Michuano ya CHALENJI CUP ambako walikuwa Kundi C baada ya
kutoka sare 0-0 na Zanzibar, kufungwa 3-2 na Malawi na 2-0 na Rwanda.
Mwaka 2010,
kwenye Michuano ya CECAFA Nchini Tanzania, Wachezaji 13 wa Eritrea waliyeyuka na
hatimae kubambwa na kuomba Hifadhi ya Kisiasa na baadae kupelekwa huko Houston,
Marekani chini ya Programu ya Wakimbizi.
Sasa hii
inakuwa desturi sugu ya nchi hiyo kuzamia nchi za watu wanapokwenda kwenye
mashindano, kwani awali wachezaji wanne walizamia walipokwenda kucheza na
Tusker nchini Kenya kwenye Ligi ya Mabingwa mwaka 2006 mjini Nairobi na wengine
zaidi Waliwahi kuzamia pia walipokwenda Angola mwaka 2007 kucheza mechi ya
kuwania kufuzu Fainali za Kombe la Dunia.
Timu hiyo
ilifanya hivyo hivyo mwaka 2009 nchini Kenya na katika kambi nzima alibaki
kocha na mchezaji mmoja tu. Kutokana na mfululizo wa matukio hayo, walijitoa
kwenye mashindano ya kimataifa mwaka 2010 na mashindano ya mwaka huu ya
Challenge ndio ya kwanza kushiriki baada ya kurudi.
Serikali ya
Eritrea ilisema ili kudhibiti tabia hiyo, kila mchezaji atatakiwa kuweka bondi
fedha za nchi hiyo 100,000 kabla ya kusafiri kwenda kuiwakilisha nchi, lakini
hiyo nayo inaonekana bado haijawa tiba.
No comments:
Post a Comment