Tusherehekee sikukuu za krisimas na mwaka mpya kwa Amani,Ushirikiano,Furaha na Upendo. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Monday, December 24, 2012

Tusherehekee sikukuu za krisimas na mwaka mpya kwa Amani,Ushirikiano,Furaha na Upendo.

Wakristu nchini leo(Desemba 25,2012) wanaungana na wenzao duniani katika kuadhimisha sikukuu ya X-mass.

 

Sikukuu hiyo ni kumbukumbu ya tukio la kuzaliwa kwa yesu kristu ambalo lilitokea zaidi ya miaka 2000 iliyopita katika bethlehemu ya Uyahudi.



Mkuu wa jeshi la polisi wilayani Ngara mkoani Kagera Bw Mohamed Milanzi  amewataka viongozi na wananchi kutoa ushirikiano kwa jeshi hilo ili kuimarisha usalama katika kipindi cha sikukuu za krismas na mwaka mpya. 



OCD Milanzi ameagiza wakuu wa vituo, na askari wa usalama barabarani kuhakikisha usalama unaimarika katika wilaya hiyo pamoja na kuwataka  viongozi na wananchi kutoa taarifa za watu ambao wataonekana kusababisha uvunjifu wa amani ili hatua zichukuliwe.



OCD Milanzi  amewatahadharisha madereva wa vyombo vya moto kuacha kuendesha   wakiwa wamelewa ili kuepuka ajali.



Blog ya Mwana wa Makonda nawatakia wasomaji wetu wote sikukuu njema ya X-mass na Mwaka mpya wa 2013.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad