Simu za mkononi husababisha watoto kuzaliwa watukutu, uharibifu wa manii, mimba, kupungua kwa nguvu za kiume na kupoteza kumbukumbu. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Wednesday, December 05, 2012

Simu za mkononi husababisha watoto kuzaliwa watukutu, uharibifu wa manii, mimba, kupungua kwa nguvu za kiume na kupoteza kumbukumbu.


Mionzi ya simu za mkononi inaweza kuathiri maendeleo ya ubongo wa watoto walioko tumboni mwa mama zao, utafiti umeeleza.Utafiti huo umetaja madhara mengine ya mionzi ya simu za mkononi kuwa ni uharibifu wa manii, mimba, kupungua kwa nguvu za kiume, kupoteza kumbukumbu na kuzaa watoto watukutu.



Pia umeeleza kuwa matumizi kupita kiasi ya simu hizo, husababisha mtindio wa ubongo na upungufu wa udadisi kwa watoto tangu udogo wao.


Hata hivyo, utafiti huo uliofanywa na Shule ya Tiba na Dawa ya Chuo Kikuu cha Yale, Marekani na kuripotiwa na Gazeti la The Telegraph la Uingereza, umepingwa na watafiti wengine, wakisema haujakidhi baadhi ya vigezo ili kuuthibitisha.



Kiongozi wa jopo la utafiti huo, Profesa Hugh Taylor alisema utafiti huo ulioanzia kwa panya, baadaye ulithibitika kwa binadamu.



 Meneja wa Mawasiliano wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Innocent Mungy alisema utafiti huo unaweza kuwa msaada mkubwa kwa nchi kama Tanzania ambayo hivi sasa ndiyo imechipukia katika matumizi ya simu za mkononi.



No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad