Cristiano Ronaldo arudi Old Trafford dhidi ya Manchester United FC akiwa Real Madrid CF katika hatua ya 16-Bora ya Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya huku Lionel Messi wa Barcelona akiwakabili AC Milan ya Italia. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Thursday, December 20, 2012

Cristiano Ronaldo arudi Old Trafford dhidi ya Manchester United FC akiwa Real Madrid CF katika hatua ya 16-Bora ya Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya huku Lionel Messi wa Barcelona akiwakabili AC Milan ya Italia.

UEFA CHAMPIONS LEAGUE
Droo ya Raundi ya Mtoano ya Timu 16 ya UEFA CHAMPIONS LEAGUE imefanyika leo huko Nyon, Nchini Uswisi na kutoa Mechi zenye mvuto wa aina yake kwa Wadau wa Soka ambapo Mechi za kwanza za Raundi hiyo zitachezwa Tarehe 12 na 20 Februari 2013 na marudiano ni Machi 5 na 13.


 

CRISTIANO Ronaldo atarejea Manchester United akiwa na mabingwa mara tisa Real Madrid katika mechi ya hatua ya 16-Bora ya Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya huku Lionel Messi wa Barcelona akiwakabili AC Milan ya Italia.



Bayern Munich  ambao msimu uliopita walifungwa katika fainali na Chelsea, watacheza dhidi ya Arsenal wakati Juventus itaikabili timu ambayo haikutarajiwa kufika hatua hiyo ya Celtic




Timu inayotumia pesa nyingi kusajili wachezaji ya Paris St Germain itacheza dhidi ya Valencia.



Lakini ratiba ya miamba wawili wa Hispania ndiyo iliyovutia tukio hilo la leo katika makao makuu ya UEFA na wote wawili walipangiwa timu ambazo ni mabingwa wa zamani wa Ulaya.



Manchester United
Real Madrid  mabingwa wa Hispania, wamekuwa na msimu mbaya kwenye La Liga msimu huu na walimaliza wakiwa wa pili katika kundi lao la Ligi ya Klabu Bingwa nyuma ya Borussia Dortmund.



Lakini Ronaldo atakuwa na hamu kubwa ya kuiinua  timu yake ya Madrid dhidi ya klabu yake ya zamani aliyoiongoza kutwaa ubingwa huo wa Ulaya mwaka 2008 na ambayo ilimsaidia kuwa mshambuliaji wa kiwango cha dunia na pia  katika uwanja wa Old Trafford Jijini London Uingereza  kwa mara ya kwanza tangu ahame hapo na kwenda Real Madrid Mwezi Juni Mwaka 2009 kwa Dau la Pauni Milioni 80.




Kocha wa Real, Jose Mourinho, ambaye aliwahi kuifundisha Chelsea, pia atakumbana na hasimu wake wa zamani Alex Ferguson.



"Ninaamini itakuwa mechi 'spesho' kwake (Ronaldo)," alisema Emilio Butragueno, mkurugenzi wa mahusiano wa Real Madrid. "Nadhani mashabiki watakuwa na furaha kubwa, kubwa sana kwa mechi hii itakayokuwa na mvuto wa aina yake.



"Itakuwa kitu kizuri kwa kila mmoja."




Barcelona Tito Vilanova
FC Barcelona hivi sasa wanapewa nafasi kubwa ya kutwaa ubingwa wa Ligi ya Klabu Bingwa msimu huu lakini wamepangiwa timu yenye mafanikio makubwa zaidi yao katika michuano hiyo ya Ulaya AC Milan ambayo imetwaa ubingwa huo mara saba wakati michuano hiyo itakaporejea katikati ya Februari.




Messi amefunga magoli 90 mwaka 2012 ameiongoza Barcelona kukaa kileleni mwa msimamo wa La Liga kwa tofauti ya pointi tisa wakati Milan wako pointi 14 nyuma ya vinara Juventus katika mbio za ubingwa Ligi Kuu ya Italia (Serie A) na walimaliza wa pili nyuma ya Malaga katika kundi lao.



Makamu wa rais wa Barcelona, Josep Maria Bartomeu aliiambia televisheni ya Hispania ya Canal Plus: "Milan ni moja ya klabu kubwa za Ulaya na ni timu ambayo inaheshima kubwa.




"Hawafanyi vyema hivi sasa katika ligi yao lakini wana wachezaji wazuri. Hawako katika kiwango chao cha juu kwa sasa lakini soka hubadilika siku moja kwenda nyingine."



Katika mechi nyingine, Galatasaray watacheza dhidi ya Schalke 04, Shakhtar Donetsk watawakabili Dortmund na Porto watawavaa Malaga.




Ratiba ya Ligi ya 16-Bora Klabu Bingwa Ulaya iliyopangwa  mjini Nyon Nchini  Uswisi: 

 


Galatasaray                v    Schalke 04

Celtic                           v   Juventus

Arsenal                       v   Bayern Munich

Shakhtar Donetsk    v   Borussia Dortmund

AC Milan                    v   FC  Barcelona

Real Madrid              v    Manchester United

Valencia                     v   Paris St Germain

Porto                           v     Malaga   


 

*Washindi wa pili wa hatua ya makundi wanaanzia nyumbani. 


* Mechi za kwanza zitachezwa Feb 12/13 na 19/20, za marudiano zitapigwa Machi 5/6 na 12/13.


EUROPA LEAGUE
LAST 32 DRAW
BATE Borisov VS Fenerbahce
 Inter VS CFR Cluj
 Levante VS Olympiakos
 Zenit St Petersburg VS Liverpool
 Dynamo Kiev VS Bordeaux
 Bayer Leverkusen VS Benfica
 Newcastle United VS  Metalist Kharkiv
 Stuttgart VS Genk
 Atletico Madrid VS Rubin Kazan
Ajax VS  Steaua Bucharest
 Basel VS  Dnipro
 Anzhi VS Hannover
 Sparta Prague VS Chelsea
 Borussia Monchengladbach VS Lazio
Tottenham VS Olympique Lyonnais
 Napoli VS Viktoria Plzen

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad