Askari polisi wawili wamewaua na Wananchi wa Kata ya Mugoma, Wilaya ya Ngara mkoani Kagera na kuchoma moto Kituo cha Polisi Mugoma kwa madai kuwa polisi hao wamemuua kwa kumpiga risasi mwananchi mwenzao bila hatia. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Sunday, December 16, 2012

Askari polisi wawili wamewaua na Wananchi wa Kata ya Mugoma, Wilaya ya Ngara mkoani Kagera na kuchoma moto Kituo cha Polisi Mugoma kwa madai kuwa polisi hao wamemuua kwa kumpiga risasi mwananchi mwenzao bila hatia.


Kituo cha police Mugoma wilayani Ngara

mkoani Kagera kikiwa kimechomwa

moto na wananchi,baada

ya asikari police kumuua

mkazi mmoja kwa risasi

na hivyo kusababisha vurugu

zilizopelekea askari

wawili kufariki dunia.
Vitendo vya wananchi kujichukulia sheria mikononi vinaendelea kushika kasi ambapo askari wawili wa Jeshi la Polisi Wilaya ya Ngara mkoani Kagera, wanadaiwa kuuwawa  na wananchi wenye hasira kali jana.



Taarifa kutoka eneo la tukio zinasema kuwa mauaji hayo yalifanyika baada ya wananchi hao kuvamia na kukichoma moto kituo cha polisi cha Mugoma wilayani humo baada ya askari hao kudaiwa kumpiga risasi fundi wa pikipiki.



Kwa mujibu wa mashuhuda, tukio hilo lilitokea mchana wakati askari kadhaa wa kitengo cha usalama barabarani walipofika kwa fundi pikipiki huyo na kutaka kuichukua pikipiki aliyokuwa akiitengeneza kwa madai kuwa ilikuwa na makosa.



Fundi huyo aligoma na kueleza kuwa asubiriwe mwenye pikipiki ili kuepuka kudaiwa chombo hicho cha usafiri.



Mashuhuda hao, walidai kuwa baada ya mvutano wa muda mfupi, askari hao walifyatua risasi na kumpiga fundi huyo mguuni na kifuani, hivyo kusababisha kifo chake.



Aliongeza kuwa, tukio hilo liliwapandisha hasira wananchi na kuwafukuza askari hao waliokimbilia katika kituo hicho cha polisi.



Wananchi hao waliamua kukichoma moto kituo hicho hatua iliyosababisha askari waliokuwemo kutoka na kukimbia kila mmoja na muelekeo wake.



Alisema kuwa askari aliyetajwa kwa jina la Koplo Paschal alianguka wakati akijinusuru, hivyo kuvamiwa na wananchi waliokuwa na zana mbalimbali za jadi ambazo walitumia kumshambulia na kumuua papo hapo.



Wananchi hao pia wanadaiwa kumfuata askari mwingine anayetajwa kwa jina la Pc Alex aliyekuwa amekimbilia kwenye nyumba ya mwananchi mmoja na kumtoa kwa nguvu na kisha kuanza kumshambulia hadi kumuua.



Tukio hilo limetokea ikiwa ni siku ya soko katika eneo hilo la Mugoma linalopakana na nchi jirani ya Burundi ambapo raia wa Tanzania na Burundi hukutana na kufanya biashara jirani na kituo hicho cha polisi.




IGP Said Mwema. 

Aidha wamiliki wa maduka katika eneo hilo  la Mugoma wilayani Ngara mkoani Kagera wamesita kufungua biashara zao kwa kile kinachodaiwa kuwa ni kuogopa msako unaoendeshwa na askari wa Jeshi la Polisi kufuatia tukio hilo la hapo .  

 

Diwani wa kata ya Mugoma Bw George Rubagora ameiambia radio kwizera kuwa wakazi  wa eneo hilo wamekumbwa na hofu kutokana na  kukamatwa kwa watu wengi wakidaiwa kuhusika kwenye tukio hlo na kwamba imewapelekea baadhi ya wakazi  wa kata ya Mugoma Kukimbilia nchi jirani wakihofia kukamatwa.



Kutokana na kuchomwa moto kwa kituo hicho, nyaraka mbalimbali zinadaiwa kuteketea, huku pikipiki na baiskeli kadhaa zilizokuwa kituoni hapo nazo zikiteketea.



Mkuu wa Wilaya ya Ngara, Costa Kanyasu naye alithibitisha vifo vya askari hao na kueleza kuwa wanaendelea kufanya uchunguzi kujua ukweli wa tukio hilo, ikiwa ni pamoja na kujua kama askari hao ndiyo walimpiga risasi mwananchi huyo.





Katika hatua nyingine mkuu wa wilaya ya Ngara Bw Costantine Kanyasu amelitaka jeshi la Polisi kutumia weledi katika kuendesha msako huo kwa kuepuka kuwakamata wasiohusika kwenye matukio hayo pamoja na kuwataka wanasiasa kuepuka kutoa maneno ya uchochezi wakati huu msoko ukiwa unaendelea.



Aidha mpaka sasa Watu 18 wanashikiliwa na jeshi la Polisi wakituhumiwa kuhusika na tukio hilo la mauaji ya askari polisi wawili pamoja na kuchoma moto kituo cha polisi cha Mugoma wilayani Ngara mkoani kagera .

 


Kamanda wa Polisi wa mkoa wa Kagera Bw Philipo Karangi amesema watu hao 18 wamekatwa katika msako unaoendelea kufanyika ili kuwabaini waliohusika katika matukio hayo .

1 comment:

Post Bottom Ad