![]() |
Hili ni Basi
la Dar Express kutoka Arusha kwenda Dar linateketea kwa moto eneo la Segera,
mkoani Tanga, abiria wote 65 wamenusurika. Picha zote na Tanga Yetu Blog.
|
Aidha
huko Mkoani Shinyang’a ,idadi ya watu
waliofariki katika ajali ya gari iliyohusisha basi la abiria mali ya kampuni ya
KRF na lori la mizigo katika kijiji cha Ngongwa wilayani Shinyanga, imeongeza
na kufikia watu wane.
Kaimu
kamanda wa polisi wa mkoa wa shinyanga Bw Onesmo Ryanga, amesema idadi ya watu
waliojeruhiwa katika ajali hiyo imefikia 26 hadi sasa.
Awali
akithibitisha kutokea kwa ajili hiyo kaimu kamanda huyo wa polisi amesema, basi
lililohusika katika ajali hiyo linafanya safari zake kati ya Dar es salaam na
Bukoba.
Bw
Ryanga amesema, ajali hiyo imetokea leo majira ya saa kumi na mbili asubuhi katika eneo la barabara ya Kahama kuelekea
Bukombe.
![]() |
Hivi ndivyo picha za ajali ya mbalizi mbeya magari yakiwaka moto baada ya kugongana leo na kusababisha vifo vya watu kumi. |
No comments:
Post a Comment