![]() |
| Mwili wa
Marehemu Daudi ukiwa chini baada ya kulipukiwa na bomu. |
![]() |
|
Marehemu Daudi
|
Mwandishi wa
habari na Mwenyekiti wa Chama cha Waandishi wa Habari Mkoa wa Iringa (IPC),
Daudi Mwangosi amefariki dunia kwenye kijiji cha Nyololo, Mufindi, Iringa baada
ya kutokea vurugu kati ya polisi na wafuasi wa chama cha Chadema.
Mwangosi
ambae ni mwandishi wa habari wa kituo cha Televisheni cha Channel ten,
amefariki papo hapo kwenye eneo la tukio ambapo vurugu zilitokea katika kijiji
cha Nyololo wilaya ya Mufindi mkoani Iringa september 2, 2012 saa kumi jioni
katika ofisi za Chadema Nyololo huku askari mmoja akijeruhiwa kwa risasi .
Kabla ya
kifo chake, mabomu yalipigwa eneo hilo ili kuwatawanya wafuasi wa Chadema ambao
walikuwa wakigoma kutawanyika.
Chanzo cha
mwanahabari Mwangosi kuuwawa kilitokana na kukamatwa kwa mwandishi wa habari wa
gazeti la Nipashe mkoa wa Iringa Godfrey Mushi na hivyo mwanahabari huyo
alitaka kuhoji polisi sababu ya kukamatwa kwa mwanahabari huyo ndipo askari hao
walipoanza kumshambulia kwa kipigo na baadae mlio kama wa bomu ulisikika eneo
hilo ambapo mwandishi huyo pamoja na askari mmoja wakaanguka chini .
![]() |
|
Gari la
Chadema lililovunjwa kioo wakati wa vurugu.
|
Ndani ya
dakika tano ilisikika sauti ya askari huyo ikisema afande nimekufa ndipo
walipomchukua na kumpeleka Hospitali ya wilaya ya Mufindi huku mwili wa mwanahabari
huyo ukipelekwa chumba cha kuhifadhia maiti .
Katika
vurugu hizo zilizodumu kwa dakika 30 kwa askari na wafuasi wa Chadema
kurushiana mawe na mabomu, zaidi ya magari matano ya Chadema na ya wananchi
yameharibiwa huku watu kadhaa wakijeruhiwa akiwemo mwanahabari mmoja Godfrey
Mushi.
![]() |
|
Mwandishi
David mwenye sweta la rangi ya udongo akipiga picha nusu saa kabla ya kifo
chake.
|














No comments:
Post a Comment