Watu watatu wametekwa katika pori la Kanembwa wilayani Kibondo mkoani Kigoma kasha kujeruhiwa kwa risasi. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Friday, August 31, 2012

Watu watatu wametekwa katika pori la Kanembwa wilayani Kibondo mkoani Kigoma kasha kujeruhiwa kwa risasi.

Watu watatu wamejeruhiwa kwa risasi baada ya kutekwa na watu wasiojulikana katika pori la kanembwa wilayani Kibondo mkoani Kigoma na wawili kati yao wamelazwa katika hospitali ya wilaya ya Kibondo .



Waliotekwa ni Josephat Maimu, Shukuru Benet na Noel Godfrey ambao walikuwa wakisafiri kuelekea kahama katika shughuli za kawaida .



Mmoja wa majeruhi hao Josephat Maimu amesema kabla ya tukio hilo kutokea aliona magari mawili yakiwa yamesimama na kudhani kuwa magari hayo yalikuwa yameharibika.



Josephat Maimu akiwa katika hospitali ya wilaya kibondo baada ya kujeruhiwa na majambazi katika poli la kanembwa kibondo (picha na james jovin).



 Muuguzi wa zamu katika hospitali ya wilaya ya kibondo Bi Christina Samizi amesema majeruhi hao wanaendelea kupata matibabu.  




No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad