Watu watatu wamejeruhiwa kwa risasi baada ya kutekwa
na watu wasiojulikana katika pori la kanembwa wilayani Kibondo mkoani Kigoma na
wawili kati yao wamelazwa katika hospitali ya wilaya ya Kibondo .
Waliotekwa ni Josephat
Maimu, Shukuru Benet na Noel Godfrey ambao walikuwa wakisafiri kuelekea
kahama katika shughuli za kawaida .
Mmoja wa majeruhi hao Josephat Maimu amesema kabla ya tukio hilo kutokea aliona magari
mawili yakiwa yamesimama na kudhani kuwa magari hayo yalikuwa yameharibika.
Josephat Maimu akiwa katika
hospitali ya wilaya kibondo baada ya kujeruhiwa na majambazi katika poli la
kanembwa kibondo (picha na james jovin).
|
Muuguzi wa zamu katika
hospitali ya wilaya ya kibondo Bi Christina Samizi amesema majeruhi hao
wanaendelea kupata matibabu.
No comments:
Post a Comment