Mwanamke
aliyetiwa mbaroni akificha sura yake
wakati akitoka mahakamani.
|
Mwanamke mmoja mkazi wa Pretoria nchini Afrika Kusini amepandishwa
kizimbani kwa tuhuma za ukatili kwa wanyama baada ya kugundulika kuwa kwa muda
mrefu amekuwa akifanya mapenzi na mbwa wake wawili.
Mwanamke huyo mzungu mwenye nywele za hudhurungi
alitiwa mbaroni siku ya jumatatu baada ya malalamiko ya mwanamke huyo kufanya
mapenzi na mbwa kupelekwa kwenye taasisi ya kulinda wanyama.
Kwa mujibu wa vyanzo vya polisi, mtu mmoja ambaye
hakutaka kugundulika alipeleka DVD ya mwanamke huyo akifanya mapenzi na mbwa
kwenye taasisi ya kutetea haki za wanyama ambayo iliamua kupeleka suala hilo
polisi.
Polisi walipewa kibali cha kuisachi nyumba ya
mwanamke huyo ambapo DVD nyingi sana za mwanamke huyo akifanya mapenzi na mbwa
zilipatikana.
"Inavyoonekana alikuwa akirekodi video za
mapenzi yake na mbwa kwa muda mrefu sana. Alitiwa mbaroni muda mfupi baada ya
nyumba yake kusachiwa", kilisema chanzo cha polisi.
Mwanamke huyo alipandishwa kizimbani siku ya
alhamisi ambapo hakimu aliamuru mwanamke huyo apimwe akili zake kabla ya kesi
hiyo haijaendelea zaidi.
Akitoka mahakamani baada ya kulipiwa dhamana na
rafiki yake wa kiume, mwanamke huyo alijificha sura yake kwa kutumia gazeti ili
waandishi wa habari wasimpige picha.
Mbwa waliokuwa wakifanya mapenzi na mwanamke huyo
wamechukuliwa na kupelekwa sehemu nyingine kwa uchunguzi zaidi.
Chanzo: nifahamishe.com
No comments:
Post a Comment