Mahakama kuu divisheni kazi yabatilisha mgomo wa walimu nchini. - Mwana Wa Makonda
cV7ufzj

Muhtasari

X-BET

MAIN-

Post Top Ad

cV7ufzj

Friday, August 03, 2012

demo-image

Mahakama kuu divisheni kazi yabatilisha mgomo wa walimu nchini.

.com/simgad/
385379_477758745584974_1874304159_n

Mwanafunzi anapoamua kuchukua nafasi ya ualimu. Hakika hapa ndipo inapoonekana walimu ni watu/walezi muhimu sana.


Mahakama kuu divisheni kazi leo imebatilisha mgomo wa walimu nchini uliokuwa ukiendelea kwa lengo la kushinikiza serikali ili kuboresha masilahi yao.

 


Hatua hiyo imekuja baada ya serikali kufungua kesi mahakamani ikitaka mgomo huo ubatilishwe.

 

 

Makama kuu divisheni ya kazi imesema mgomo ulioitishwa na chama cha walimu CWT haukuwa halali hivyo kuamuru walimu wote kurejea kazini.

 


tisa

Kufuatia tamko hilo la mahakama katibu wa chama cha walimu wilaya ya  Ngara  mkoani Kagera Bw Vedastus Nsinde akawataka walimu wote wilayani Ngara kesho August 3, 2012 kuendelea na kazi kama kawaida wakati taratibu nyingine zikiendelea.

 

 

Tangu July 30 mwaka huu walimu waligoma wakishiniki serikali kuboresha masilahi na mazingira bora ya kazi.


B

Walimu wamegome je sisi wanafunzi tufanyeje?? Kumbukeni kuwa sisi tuna haki ya kupata ELIMU.

 

8E9U8966

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiongea na wahariri Ikulu jana.

Aidha hapo Jna katika Hotuba yake Rais Jakaya Mrisho Kikwete aliwahakikishia  walimu kuwa tunawajali, tunawathamini na kutambua mchango wao muhimu kwa taifa letu.  

 

 

 â€˜â€™Wakati wote tumekuwa tunashughulikia madai ya haki zao na malimbikizo mbalimbali.  Madai ya safari hii ni makubwa mno, yametuzidi kimo.  Athari za kuyatimiza yalivyo yataifanya bajeti ya Serikali kutumia asilimia 75 kwa ajili ya mishahara ya watumishi wa Serikali na kubakiza asilimia 25 kwa kuendeshea Serikali na kutimiza majukumu ya maendeleo kwa wananchi.  Haitakuwa sawa. ‘’

 

 

 Ndiyo maana tumeshindwa kuelewana walipokataa rai hiyo na wao kusisitiza kugoma hivyo aliwasihi warudi kwenye meza ya mazungumzo.


No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad

Contact Form

Name

Email *

Message *