Mabilioni ya wasanii yaibwa kupitia Sekta ya Mawasiliano - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Thursday, July 26, 2012

Mabilioni ya wasanii yaibwa kupitia Sekta ya Mawasiliano

Mbunge  wa Kigoma Kaskazini, Kabwe Zitto (CHADEMA),akiwa na Wasani wa kundi la Kigoma Allstarz.


Mbunge  wa Kigoma Kaskazini, Kabwe Zitto (CHADEMA), amesema Kampuni ya mtandao ya Onmobile inashirikiana na makamupni ya simu za mikononi kuwanyonya wasanii kwa kuwalipa asilimia ndogo ya mapato yanayotokana na matumizi ya nyimbo zao.


Akichangia hotuba ya bajeti ya Wizara ya Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia iliyosomwa bungeni mjini Dodoma jana, Zitto alisema kinachoshangaza kampuni hiyo iliyohodhi mambo yote ya kampuni za Vodacom na Airtel, inafanya kazi bila leseni.


“Ukimpigia simu Waziri Mkuu… utasikia simu yake ina wimbo wa Rose Mhando, Naibu Waziri Adam Malima yeye upo wimbo wa Dar mpaka Moro wa Wanaume Familly na ukinipigia mimi utasikia Kurani ama wimbo wa CHADEMA.


“Lakini kinachoshangaza wasanii hawa wananyonywa licha ya nyimbo zao kutumika, tunadhani wasanii wanapata… si kweli kwani hata vituo vya redio na televisheni vya serikali vinatumia nyimbo hizi bila kuwalipa chochote.


Zitto alipendekeza kuwa, wakala huyo afukuzwe nchini kwa kuisababishia nchi hasara na kushauri kipato cha wasanii kupitia nyimbo zinazotumika kwenye miito ya simu kiongezwe hadi asilimia 50 ili kuwawezesha kujikimu kimaisha.


“Wasanii wapate haki yao na walipwe kutokana na jasho lao. Kazi ya dola ni kumlinda mnyonge. Kampuni za simu ni giant (kubwa), ukiwauliza wanasema hawana mkataba na wasanii. Kwa nini kampuni hiyo ifanye kazi bila leseni?” alihoji.


Imani ni nguvu inayoishi, ‘’imani ni kuwa na hakika ya mambo yatarajiwayo ni bayana ya mambo yasiyoonekana>> hivyo >> MWENYE HAKI ATAISHI KWA IMANI (HABAKUKI 2:4)


Nyimbo hizo ni zile ambazo mteja wa mtandao husika, huomba ili akipigiwa simu asikie wimbo huo na huduma hiyo hutozwa Sh300 kwa kila wimbo.


Uchunguzi ulibaini kuwa, kila siku Kampuni ya Airtel hupata Sh15 milioni huku Vodacom wakipata karibu Sh20 milioni kutokana na bishara hiyo.


Makampuni makubwa ya Vodacom na Airtel wameingia mkataba na Onmobile na wanaingiza sh bilioni 43 kutokana na milio,” alisema mbunge huyo aliyeonyesha nia ya kuutaka urais mwaka 2015 kupitia chama chake.



Mkurugenzi Mkuu wa TCRA, Profesa John Nkoma alilieleza gazeti hili kuwa, alikuwa hafahamu kwamba Kampuni ya Onmobile ilikuwa ikifanya kazi nchini, kwani awali waliipa masharti ambayo ilipaswa kuyatimiza kabla ya kupewa leseni.


Aliyataja masharti hayo kuwa ni pamoja na kueleza zilipo ofisi zao nchini kutaja wanahisa wao; shughuli wanayotaka kuifanya pamoja na mambo mengine.


Kuhusu ushiriki wa Vodacom na Airtel katika biashara hiyo Profesa Nkoma alisema: “Sina taarifa kama wanafanya kazi. Unachotakiwa kufanya, zungumza na Airtel na Vodacom wakueleze kwa nini wanafanya kazi na kampuni ambayo haina leseni.”


Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, January Makamba


Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, January Makamba akijibu hoja za wabunge jana jioni alisema kuwa, tayari Serikali imeizuia Kampuni ya Onmobile kutoa huduma kutokana na kutokuwa na usajili kisheria.


“Kampuni hii iliomba kibali cha kufanya kazi hii Februari 29, mwaka huu pale TCRA, lakini ukweli ni kuwa, ilinyimwa kwa sababu haikuwa na usajili wa Brela,” alisema Makamba.



Kuhusu wizi wa kazi za wasanii, naibu waziri huyo alisema umekuwa ukifanywa pia kwa njia mbalimbali ikiwa ni pamoja na kutopata mrabaha nyimbo zao zinapochezwa redioni na kwenye televisheni.


No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad