Fainali ya KAGAME CUP 2012 / 2013 ni Yanga v Azam!! - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Thursday, July 26, 2012

Fainali ya KAGAME CUP 2012 / 2013 ni Yanga v Azam!!

Kikosi cha Azam FC

Timu za  Tanzania, Mabingwa watetezi  Yanga na Azam FC , leo zimeshinda Mechi zao za Nusu Fainali za mashindano ya kombe la Kagame , Kombe la Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati, na kutinga Fainali ambayo inahakikisha Kombe hilo litabaki Tanzania.

Katika Nusu Fainali ya kwanza, bao la Dakika ya 89 la Supastraika  Mrisho Ngassa liliwapa Azam FC ushindi wa bao 2-1 dhidi ya Vita Club ya Congo DRC  katika Mechi ambayo Azam FC  walitanguliwa kufungwa katika Dakika ya 34.

Kipindi cha pili pasi ya Tchetche iliunganishwa vyema na Bocco aliefunga bao la kusawazisha katika Dakika ya 68 na Mchezaji alietoka benchi, Mrisho Ngassa, alimalizia pasi murua ya Salum Abukar na kupiga bao la ushindi.


Mabingwa watetezi  Yanga ‘ kilichoanza: Ally Mustapha 'Barthez', Juma Abdul, Oscar Joshua, Nadir Haroub 'Cannavaro', Kelvin Yondan, Athuman Idd 'Chuji', Godfrey Taita, Haruna Niyonzima, Said Bahanunzi, Hamis Kiiza 'Diego', David Luhende - 29

Akiba: Yaw Berko, Ladislaus Mbogo, Juma Seif 'Kijiko', Rashid Gumbo, Idrisa Rashid, Stephano Mwasika, Shamte Ally

Kwenye Nusu Fainali iliyofuatia, ngoma ilikuwa ngumu mno kati ya Yanga na APR  ya Rwanda na hadi Dakika 90 bao zilikuwa 0-0 na zikaongezwa Dakika 30 za nyongeza.

Yanga walipata bao lao moja na la ushindi katika Dakika ya 100 baada ya krosi ya Niyonzima kuunganishwa kwa kifua  na Hamisi Kiiza 'Diego'.


Kiungo Haruna Niyonzima wa Yanga. Zamani alikuwa mchezaji wa APR

Dakika 3 baadae Yanga walipata pigo pale Mchezaji wao Godfrey Taita  kuwashwa  Kadi  Nyekundu na hivyo hatacheza Mechi ya Fainali hapo Jumamosi.

 
MSHINDI WA 3:
Julai 28 Jumamosi
[Saa 8 Mchana]

Vita v APR

FAINALI:
Julai 28 Jumamosi
[Saa 10 Mchana]

Azam v Yanga

  • Rais wa baraza CECAFA, Leodegar Tenga pamoja na Katibu Mkuu wa CECAFA, Nicholas Musonye (kulia) wakiwa   katika moja ya vikao na waandishi wa habari

Katika hatua nyingine  Kombe la Kagame mwakani inatarajiwa kufanyika mapema mwezi Januari ili kuziandaa timu za Afrika Mashariki na Kati katika mashindano ya kombe la klabu bingwa na mashindano ya koombe la Shirikisho la Soka Afrika CAF.

Katibu Mkuu wa Baraza la Vyama vya Soka Afrika Mashariki na Kati (CECAFA), Nicholaus Musonye alisema wameamua hivyo baada ya kuona mapungufu makubwa katika timu za Ukanda wake hivyo mashindano ya mwaka huu yakimalizika Jumamosi Cecafa itakaa na viongozi wa vyama vya soka vya nchi husika na kuzungumza nao kuangalia namna ya kuweka mfumo mpya wa ratiba ya ligi zao.

 

 

Kauli ya Musonye imekuja baada ya Ethiopia kuyatolea nje mashindano haya ya Kagame kutokana na  Ligi Kuu ya nchi hiyo inayoendelea, wakati Tanzania imemaliza Ligi tangu mwezi Mei kitendo ambacho kinazipa wakati mgumu timu za Yanga, Azam FC na Simba.


Hata hivyo tayari makocha mbali mbali wamekuwa wakipigia kelele michuano hiyo kuwa haina tija kwa timu zinazoshiriki kwa kuwa inafanyika kukiwa hakuna michuano yoyote ya kimatafa mbeleni kitu ambacho kinazifanya timu za Ukanda wa Cecafa kuonyesha kiwango kibovu inapofika michuano inayoandaliwa na Shirikisho la Soka barani Afrika (CAF) tofauti na timu zilizopo Ukanda wa Kusini mwa Afrika (COSAFA).

 

Aidha ni lazima CECAFA  wakubali kubadilisha mfumo pamoja na kuongeza zawadi kwa washiriki wa mashindano hayo ya kombe la Kagame ili kuyapa ubora unaotakiwa.


Tangu 2002 rais wa Rwanda, Paul Kagame alipotangaza kudhamini zawadi ya washindi ya dola 60, 000, ambapo bingwa anapata dola 30,000, wakati mshindi wa pili  Dola 20,000 huku yule wa tatu anapata dola 10,000, mpaka leo zawadi hizo hazijabadilika.


Leo ni miaka kumi (10) imepita bado CECAFA haitaki kufikiria kuboresha zawadi hizo kwa washiriki pamoja na kupata wadhamini wenza.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad