![]() |
Mwanamke
aliyefahamika kwa jina la Mbonimpaye Linus mkazi wa kijiji na kata ya
Kalela wilayani Kasulu mkoani Kigoma, amefariki baada ya kuchomwa kisu tumboni
na mume wake kutokana na migogoro ya kifamilia iliyokuwepo baina yao.
Akizungumzia
tukio hilo Ndugu wa marehemu Bi. Sadasia
Linus amesema tukio hilo limetokea mwishoni mwa wiki iliyopita wakati
mwanaume huyo akimfuatilia mke wake arudi nyumbani baada ya ugomvi kutokea na
kusababisha mwanamke huyo kumkimbia mume wake na kurundi kwao.
Amesema
mwanamke huyo akiwa njiani akimsindikiza mume wake baada ya kutoka nyumbani
kwao na mwanamke, walipofika njiani alimkamata na kumchoma kisu tumboni
kilichosababisha apoteze maisha papo hapo.
Diwani wa
kata ya Kalela Bi. Dolisia Solomoni
amelaani tukio hilo na kuitaka jamii kutoa ushirikiano kwa jeshi la polisi
wakati mtuhumiwa akiendelea kutafutwa ili sheria iweze kuchukua mkondo wake.
|
Tuesday, May 22, 2018
![](https://1.bp.blogspot.com/-7Kd9qaiRHuA/WaEtZyc70TI/AAAAAAAADsA/7WUYBVoY-UwwjdEP3kDFPvH9htN0dDKgQCLcBGAs/s1600/demo-image.jpg)
Aua Mke wake kwa Kisu kisa Mgogoro wa Kifamilia -Wilayani Kasulu,Kigoma.
Tags
# HABARI
Sambaza Hii
Chief Editor | Mhariri
HABARI
Labels:
HABARI
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Kuhusu Mwandishi
Journalist / Chief Editor / Tanzanian Blogger
Simu: 0756830214 / 0620197747 / 0789925630.
No comments:
Post a Comment