![]() |
|
Mechi hiyo ya kalenda ya FIFA ilikuwa na mashambulizi ya zamu kwa timu
zote mbili haswa katika kipindi cha kwanza kilichotawaliwa zaidi na wenyeji Taifa
Stars.
Taifa Stars ilianza kuandika bao la kwanza katika dakika ya 74 kupitia kwa Mshambuliaji anayekipiga KRC Genk ya Ubelgiji, Mbwana Samatta, kufuatia kazi nzuri ya Shiza Kichuya aliyepiga krosi safi kushoto mwa Uwaja na kumkuta Samatta ambaye bila ajizi akapiga mpira kwa Kichwa. Dakika ya 86, Shiza Kichuya alioongezea Taifa Stars bao la pili kwa shuti kali la mguu wa kushoto, baada ya kutengenezewa pasi murua na Mbwana Samatta. |
![]() |
|
Ushindi huo unarejesha furaha na matumaini kwa Watanzania, baada ya
kupoteza mchezo uliopita dhidi ya Algeria kwa jumla ya mabao 4-1 ugenini.
DR Congo ni
timu bora Afrika, inashika nafasi ya tatu nyuma ya Tunisia na Senegal, ipo
nafasi ya 39 katika viwango vya Fifa vya mwezi Machi 2018 hivyo Stars imepata
matokeo dhidi ya timu bora Afrika na Duniani.
Hadi sasa
Tanzania ipo nafasi ya 146 katika viwango vya FIFA vilivyotolewa mwezi
machi 2018 ikiwa inapambana kusogea nafasi za juu kwa kucheza mechi zakirafiki
za kimataifa dhidi ya timu ambazo zipo katika nafasi za juu.
|








No comments:
Post a Comment