Rulenge Stars Bingwa wa Kombe la Polisi Jamii 2018. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Monday, March 26, 2018

Rulenge Stars Bingwa wa Kombe la Polisi Jamii 2018.

Katibu Tawala wilaya ya Ngara mkoani Geita,Vedastus Tibaijuka akimkabidhi Nahodha wa Timu ya Rulenge Stars fimbo iliyozungushiwa kamba kama zawadi ya Ng'ombe mnyama baada ya Rulenge Stars kuibuka mshindi wa Kombe la Polisi Jamii 2018 wilaya ya Ngara mkoani Kagera baada ya kuifunga Veterani FC FC ya Mjini Ngara magoli 2-0.

Rulenge Stars ya mjini Rulenge wameshinda kombe hili kwa mara ya Kwanza toka limeanzishwa na Mkuu wa Polisi wilayani Ngara Abeid Maige Jana March 25,2018 kwenye mchezo wa fainali uliochezwa uwanja wa Kokoto Mjini Ngara.
 Mkuu wa Polisi wilayani Ngara Abeid Maige akielezea mafanikio ya Kombe la Polisi Jamii 2018 kuwa yamekuza mahusiano kati ya Polisi na Jamii kupitia kauli mbiu ya KATAA UHALIFU,FICHUA WAHALIFU  na jumla ya 18 zilishiriki mashindano hayo.

Kikosi cha Mabingwa wa Polisi Jamii Cup 2018 wilayani Ngara Rulenge Stars.

Kikosi cha Veterani FC kilichofungwa na Rulenge Stars wakati wa fainali ya Polisi Jamii Cup 2018 wilayani Ngara .

Hili Kokoto aiseeee uwanjani Kokoto-uwanja wa wilaya ya Ngara mmmmmmmm''Mpira wa fainali huu , Polisi Jamii Cup 2018 wilayani Ngara.

Golikipa wa Veteran FC mtumishi wa Benki ya NMB Tawi la Ngara aliibuka Bora wa Mashindano ya Polisi Jamii Cup 2018 wilayani Ngara na kuondoka na zawadi ya fedha 20,000/. koshoto kwake ni Mkuu wa Jeshi wa Polisi wilayani humo Abeid Maige na kulia ni Vedastus Tibaijuka,Katibu Tawala wilaya.


Shuja wa mchezo huo ni Elias Jevent  ambaye aliifungia timu yake mabao hayo yote mawili na kumfanya kuibuka mfungaji bora wa mashindano kwa kufikisha mabao 7 na kuondoka na zawadi ya fedha taslimu 20,000/.

Rulenge Stars kwa Kuibuka Bingwa ,amekabidhiwa zawadi yake na Mgeni rasmi Mwenyekiti wa michezo wilaya na Katibu tawala wilaya ya Ngara mkoani Kagera Vedastus Tibaijuka Ng’ombe mnyama ,Kikombe na Mpira mmoja huku Veteran FC wakizawadiwa Mbuzi mnyama na Mpira mmoja wakati washindi wa tatu,Nyakariba FC wakizawadiwa Mbuzi mmoja na Mpira mmoja baada ya kuibuka timu yenye nidhamu.

Zawadi ya Mbuzi mnyama za Washindi wa Pili Veteran FC na Nyakariba FC washindi wa 3 wa  Polisi Jamii Cup 2018 wilayani Ngara.
Zawadi ya Bingwa wa Polisi Jamii Cup 2018 wilayani Ngara Rulenge Stars baada ya Kumfunga Veterani FC bao 2-0 katika fainali uwanja wa Kokoto Jana March 25,2018.

Mwenyekiti wa Veterani FC Jose Sinzobakwila akipokea zawadi ya mpira na mbuzi wao baada ya kuwa washindi wa pili wa Polisi Jamii Cup 2018 wilayani Ngara.



Pichani Juu Mwenyekiti wa Halmashauri na Diwani wa Kata ya Bukiriro Erick Nkilamachumu (picha ya 3 juu ) aliongoza mashabiki toka Rulenge na Kabanga kuhakikisha Rulenge wanaisapoti na wakafanikiwa kuibuka Mabingwa wa Polisi Jamii Cup 2018 wilayani Ngara.


No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad