UEFA SUPER CUP 2016:-Ni Real Madrid ikishinda 3-2 dhidi ya Sevilla.! - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Wednesday, August 10, 2016

UEFA SUPER CUP 2016:-Ni Real Madrid ikishinda 3-2 dhidi ya Sevilla.!

The Real Madrid players celebrate on Rosenborg's Lerkendal Stadium pitch after securing a European Super Cup triumph 
Mabingwa wa Ligi ya Mabingwa barani Ulaya, Real Madrid ya nchini Hispania jana usiku ,Agosti 09,2016 wameinyuka Sevilla wanaoshikilia taji la Europa  mabao 3-2 na kunyakua ubingwa wa Super Cup 2016.

Real Madrid captain Sergio Ramos celebrates with the European Super Cup trophy after clinching victory in Norway 
Real Madrid defender Dani Carvajal wheels away in celebration after scoring a dramatic last-gasp winner against Sevilla 
Real Madrid, Mabingwa wa Ulaya, wakicheza bila ya Mastaa wao wakubwa Cristiano Ronaldo, Gareth Bale, Toni Kroos na Pepe,walitangulia kufunga Bao Dakika ya 21 kwa Bao la Chipukizi Marco Asensio Willemsen aliekuwa akicheza Mechi yake ya kwanza kabisa.

Sevilla walisawazisha Dakika ya 41 kwa Bao la Franco Vazquez.
Kipindi cha pili cha mchezo huo uliopigwa kwenye dimba la Larkendal nchini Norway kilianza kwa kasi huku Sevilla wakionekana kuliandama zaidi lango la Madrid.
Sergio Ramos heads home an equaliser for Real Madrid to make it 2-2 against Sevilla in the European Super Cup  
The Spanish star defender slides on the pitch in celebration after scoring a dramatic last-gasp second-half header 
Konoplyanka aliipatia Sevilla goli la pili kwa mkwaju wa penati baada ya Sergio Ramos kufanya madhambi kwenye eneo la hatari.

Baada ya bao hilo Real Madrid waliliandama lango la Sevilla kama nyuki lakini ukuta wa mabingwa hao wa Europa ulikuwa imara kuondosha hatari zote hadi dakika 90 za mtanange huo zilipomalizika ndipo katika dakika tatu za nyongeza Ramos akaisawazishia Madrid.

Mechi hiyo ilikwenda katika muda wa nyongeza wa dakika 30 ambapo katika dakika ya 28, Danny Carvajal aliipatia Madrid bao la tatu na la ushindi hivyo kutawazwa kuwa mabingwa wa kombe hilo.
Yevhen Konoplyanka is mobbed by his Sevilla team-mates after scoring from the penalty spot in the second half
Konoplyanka, who had a disappointing Euro 2016 with Ukraine, steps up to confidently give Sevilla a 2-1 lead 
Marco Asensio watches on as the youngster's spectacular 25-yard strike opens the scoring for Real Madrid on Tuesday

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad