Benki ya NMB Kibondo yakabidhi Vitanda na Mashuka Hospitali ya Wilaya. - Mwana Wa Makonda
cV7ufzj

Muhtasari

X-BET

MAIN-

Post Top Ad

cV7ufzj

Thursday, May 17, 2018

demo-image

Benki ya NMB Kibondo yakabidhi Vitanda na Mashuka Hospitali ya Wilaya.

.com/simgad/
32782645_1862855013754400_7643140976088711168_n
Hospitali ya Wilaya ya Kibondo Mkoani Kigoma imepokea vitanda na mashuka vyenye thamani ya shilingi milioni 5 vilivyotolewa na Benki ya NMB Tawi la Kibondo katika kuunga mkono utoaji huduma bora ya afya kwa wananchi.

Meneja Kanda ya Magharibi wa Benki hiyo Bw Leoni Ngowi akizungumza katika makabidhiano hayo amesema kuwa msaada huo ni sehemu ya kile ambacho kinachangiwa na Wananchi wa wilaya ya Kibondo kupitia Benki hiyo.

Bw Ngowi amesema wanatarajia msaada huo utapunguza baadhi ya changamoto hususani za wagonjwa kukosa sehemu za kupumzika wakati wakipatiwa huduma.
32748903_1862855067087728_2040367481465339904_n
Awali akizungumzia hali ya uhaba wa vitendea kazi katika Hospitali ya wilaya hiyo, Mganga mkuu wa wilaya ya Kibondo, Dr Pima Sebastian amesema vitu hivyo vitasaidia wao kutoa huduma kwa ufasaha ikiwa ni pamoja na kupunguza swala la wagonjwa wawili kutumia kitanda kimoja.

Na –Radio Kwizera KIBONDO.
32684957_1862854980421070_5695568870098599936_n

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad

Contact Form

Name

Email *

Message *