Atletico Madrid yachukua Ubingwa wa Europa League. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Thursday, May 17, 2018

Atletico Madrid yachukua Ubingwa wa Europa League.

Furaha ya Ubingwa.

Fainali ya michuano ya UEFA Europa League msimu wa 2017/2018 imechezwa May 16,2018  mjini Lyon nchini Ufaransa na Mchezaji Antoine Griezmann ameisaidia timu yake ya Atletico de Madrid kutwaa Ubingwa wa Kombe la EUROPA League 2017/2018 kufuatia ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Marseille ya Ufaransa.

Griezmann aliweza kucheka na nyavu mara mbili katika dakika ya 21 na 49 huku moja likifungwa na Gabi kwenye dakika ya 89 ya mchezo.

Atletico Madrid walifanikiwa kuingia hatua ya fainali baada ya kuiondoa Arsenal kwa Jumla ya mabao 2-1.



Ubingwa huo sasa ni heshima pia kwa Fernando Torres ambaye ametangaza kuwa huu ndio msimu wake wa mwisho kuichezea Atletico Madrid lakini kama hufahamu tu taji hilo linakuwa ni taji la pili la Europa League kwa Atletico Madrid chini ya kocha Diego Simeone ambaye pia ameiongoza timu hiyo kufika hatua ya fainali ya Champions League na kutwaa mataji ya Copa del Rey, Super Copa, Super Cup na LaLiga.





No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad