AJALI / PICHA:-Watu Waliokufa Katika Ajali ya City Boy Wafikia 32. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Thursday, July 07, 2016

AJALI / PICHA:-Watu Waliokufa Katika Ajali ya City Boy Wafikia 32.

Idadi ya watu waliokufa katika ajali iliyohusisha mabasi mawili ya Kampuni ya CITY BOYS imeongezeka na kufikia 32 baada majeruhi aliyekuwa amelazwa katika chumba cha wagonjwa wanaohitaji uangalizi maalumu (ICU) kufariki dunia.

Ajali hiyo iliyohusisha mabasi hayo wakati moja likitokea Dar es Salaam kuelekea Kahama mkoani Shinyangana lingine likitokea Kahama kuelekea Dar es Salaam, ilitokea saa tisa Jumatatu,Julai 04,2016 katika eneo la Maweni, Kata ya Kintiku Wilaya ya Manyoni mkoani Singida.

Akizungumza jana,Julai 06,2016, Kaimu Mganga Mkuu wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Dodoma,  Dk Ibehzi Ernest alisema kazi ya kutambua miili ya marehemu hao bado inaendelea.

Alisema hadi jana miili ya watu 25 waliokufa kwenye ajali hiyo ilikuwa imetambuliwa na ndugu zao. 

Dk Ernest ambaye pia ni Daktari Bingwa wa Ajali, Upasuaji na Mifupa alisema kati ya maiti 25 zilizotambuliwa 12 zimechukuliwa na ndugu zao kwa ajili ya mazishi.

Wengine wametibiwa na kuruhusiwa tumebaki na majeruhi watano ambao hali zao zinaendelea vizuri,” alisema.

Kwa siku nzima ya juzi na jana watu walikuwa wakipishana kuwatambua ndugu zao katika chumba cha maiti cha Hospitali ya Rufaa ya Dodoma. Kutokana na miili kuharibika, ndugu hao walikuwa wakirudi mara mbili kuangalia.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad