![]() |
|
Mwenyekiti
wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Freeman Mbowe, akizungumza
wakati akitolea taarifa swala na ratiba ya Mikutano ya Kampeni za Mgombea Urais
wa Jamhuri ya Muungani wa Tanzania katika mwamvuli wa UKAWA kupitia Chama cha
Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa (kushoto) uliofanyika
kwenye Uwanja wa Kizwitwe, Sumbawanja Mjini, jana Sepremba 2, 2015.Kulia ni Mke
wa Mh. Lowassa, Mama Regina Lowassa.
|
![]() |
|
Mwenyekiti
wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Freeman Mbowe, akihutubia maelfu
ya wananchi Mkutano wa hadhara wa Kampeni, uliofanyika kwenye Uwanja wa
Kizwitwe, Sumbawanja Mjini, jana Sepremba 2, 2015 ambapo alitangaza kuanza
kampeni zake kwa kutumia helikopta (chopa) nne ambazo zitatikisa anga katika
mikoa yote nchini kuomba ridhaa ya wananchi kukichagua katika uchaguzi mkuu wa
mwaka huu.
Alisema
Tanzania nzima kuna majimbo ya uchaguzi 265 ambako Zanzibar yako 50 na Tanzania
Bara 215.
Aliongeza
kuwa siku za kampeni ni siku 60 mgombea urais Ukawa hawezi kufikia majimbo yote
hivyo Chadema imeunda vikosi vinne vya askari wa mapambano ambavyo vitaundwa na
wabunge makini na baadhi ya viongozi ambao watafanya kampeni nchi nzima kwa
kutumia helikopta nne.
Aliwataja
wabunge hao watakaounda kikosi hicho wanaomaliza muda wao kuwa ni Mbunge wa
Arusha Mjini, Godbless Lema, Ezekiel Wenje (Nyamagana), David Silinde (Momba),
Joseph Mbilinyi maarufu Sugu (Mbeya Mjini), John Mnyika (Ubungo), Halima Mdee
(Kawe) na yeye (Mbowe) ambaye ni wa Hai.
“Vikosi hivi
vitachana nchi nzima kwa kutumia helikopta kuanzia wiki ijayo, hivyo majimbo
ambayo mgombea urais hatafika vikosi vitafika na maeneo mengine atakwenda
mgombea mwenza,”alisema.
|

![]() |
|
Sehemu ya
Wananchi wa Mji wa Sumbawanga, waliofurika kwa wingi kwenye Uwanja wa Ndege wa
Sumbawanga, wakiishangilia Ndege iliyombeba Mgombea Urais wa Jamhuri ya
Muungani wa Tanzania katika mwamvuli wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na
Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa, wakati ikiwasili Uwanjani hapo,
Sepremba 2, 2015.
|
![]() |
|
Mgombea
Urais wa Jamhuri ya Muungani wa Tanzania katika mwamvuli wa UKAWA kupitia Chama
cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa na Mkewe, Mama Regina
Lowassa, wakiwapungia mikono maelfu ya wananchi wa Sumbawanga Mjini,
waliofurika kwenye Uwanja wa Kizwitwe, jana Sepremba 2, 2015.
|
![]() |
|
Mgombea
Urais wa Jamhuri ya Muungani wa Tanzania katika mwamvuli wa UKAWA kupitia Chama
cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa, akihutubia Mkutano
wa hadhara wa Kampeni, uliofanyika kwenye Uwanja wa Kizwitwe, Sumbawanja Mjini,
amesema anajua vizuri mahitaji na kero za watanzania na amewaomba watanzania
kumpa dhamana ya kuleta mabadiliko ya kweli kwani uwezo huo anao na
anachohitaji ni ushirikiano wao.
|











No comments:
Post a Comment