Sehemu ya kivuko
cha Mv Mafanikio kilichozinduliwa Rais Dkt Jakaya Kikwete mapema leo August 9,
2015 kitachofanya safari kutokea Msemo kuelekea Msangamkuu mkoani Mtwara.
PICHA NA MICHUZI JR-MTWARA.
|
Rais Kikwete
akizindua rasmi kivuko cha MV Mafanikio kwenye pwani ya mji wa Mtwara
kitachofanya safari kutokea Msemo kuelekea Msangamkuu muda huu mkoani Mtwara.
|
Mkurugenzi
Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa,Ndugu Nehemia Mchechu akizungumza jambo na
Rais Dkt Jakaya Kikwete mara baada ya
kuweka jiwe la msingi katika mradi wa ujenzi wa nyumba 30 za makazi
zinazojengwa na NHC Shangani mkoani
Mtwara zenye thamani ya shilingi bilioni 4.4,Kulia ni Waziri wa Ujenzi na
Mgombea Urais mteule wa chama cha CCM,Dkt John Pombe Magufuli wakiondoka eneo
la tukio mapema leo August 9, 2015 mchana.
|
Naibu Waziri
wa Fedha Mh.Mwigulu Nchemba akiteta jambo na Waziri wa Ujenzi Mh.John Pombe
Magufuli kabla ya uzinduzi wa Kivuko cha Mv Mafanikio mkoani Mtwara mapema leo
mchana.
|
Waziri wa
Ujenzi Dkt John Pombe Magufuli akizungumza jambo na Rais Jakaya Kikwete kabla
ya uzinduzi wa kivuko cha Mv Mafanikio mkoani Mtwara mapema leo mchana,kulia ni
Mkuu wa Wilaya ya Mtwara Mh.Fatma Salum Ali.
|
Rais Dkt
Jakaya Kikwete akizungumza jambo na Naibu Waziri wa Fedha,Mh Mwigulu Nchemba
ambaye pia alihudhuria sherehe hizo fupi uzinduzi wa kivuko cha Mv Mafanikio
mkoani Mtwara mapema leo August 9, 2015 mchana.
|
Rais
Dkt.Jakaya Kikwete akiwapungia mkono wananchi wa Msanga Mkuu-Mtwara vijijini
waliofika kwenye uzinduzi wa kivuko cha MV Mafanikio chenye uwezo wa kubeba
watu 100 na magari sita,chenye jumla ya thamani ya shilingi bilioni 3.3.
|
Waziri wa
Ujenzi na Mgombea Urais wa chama cha Mapinduzi,Dkt Jonh Pombe Magufuli
akizungumza jambo mbele ya wananchi wa Msanga Mkuu-Mtwara vijijini baada ya
uzinduzi wa kivuko cha MV Mafanikio
chenye uwezo wa kubeba watu 100 na magari sita,chenye jumla ya thamani ya
shilingi bilioni 3.3,Dkt Magufuli amesema kuwa Rais Jakaya Kikwete katika utawala
wake ndani ya maiaka kumi amefanikiwa kujenga vivuko vipya 15 na vingine 7
vimekwishakarabatiwa na vinafanya kazi mpaka sasa.
|
Rais
Dkt.Jakaya Kikwete akizungumza jambo mbele ya wananchi wa Msanga Mkuu-Mtwara
vijijini kuzindua kivuko cha MV Mafanikio chenye uwezo wa kubeba watu 100 na
magari sita,chenye jumla ya thamani ya shilingi bilioni 3.3.
|
Mkuruegenzi
Mkuu wa NHC,Nehemia Mchechu akizungumza jambo mbele ya mgeni rasmi Rais Dkt
Jakaya Kikwete pamoja na viongozi mbalimbali wa serikali na wananchi kwa ujumla
katika mradi wa ujenzi wa nyumba 30 za makazi zinazojengwa na NHC Shangani mkoani Mtwara zenye thamani
ya shilingi bilioni 4.4.
|
PICHA NA MICHUZI JR-MTWARA.
No comments:
Post a Comment