|
January
Makamba ameandika kupitia ukurasa wake wa Facebook kuwa,’’-Mwanza mmetia fora
sana kwa mapokezi yenu, hamasa na udhamini wenu siku ya juzi June 20,2015!
Asanteni sana kwa
kuitikia wito na kujiunga na kampeni yetu. Huu ni wakati wa kizazi cha sasa
kujenga #TanzaniaMpya ya miaka 50 ijayo.
Aina ya uongozi tutakaouchagua mwaka huu ndio utaamua mustakabali wa nchi yetu.
Baada ya miaka 50 ya uongozi wa kizazi kilichopita, sasa ni wakati wa nchi yetu
kuongozwa na viongozi wa aina mpya, wenye mtazamo mpya, fikra mpya, maarifa mapya na majawabu mapya.
Na
niko tayari kutengeneza na kuongoza timu madhubuti ya Watanzania wazalendo na
waadilifu watakaounda Serikali itakayojenga kesho njema. Tunayo dhamira na
uwezo wa kushinda na kuongoza mabadiliko makubwa ambayo Watanzania
wanayatarajia.
|
No comments:
Post a Comment