![]() |
Basi dogo la
abiria aina ya Toyota Hiace liliua Watu 7 papo hapo na wengine 8 kujeruhiwa.
|
![]() |
Muonekano wa
Lori aina ya Fuso lenye namba za usajili T 621 ATD lililokuwa limepakia
matofali likiwa limeharibika vibaya baada ya Basi dogo la abiria aina ya Toyota
Hiace.
|
Watu 7
wamefariki na wengine 8 kujeruhiwa baada ya magari mawili kugongana katika eneo
linalofahamika kama Ziro Ziro yaliyopo makutano ya Barabara ya kutoka wilayani Ngara
kuelekea Nyakahura na ile iendayo nchini Rwanda kupitia Benaco .
Jeshi la
polisi wilayani Ngara limesema kuwa ajali hiyo iliyotokea leo(Agosti 08,2013) mchana na kulihusisha basi dogo la abiria aina
ya Toyota Hiace lenye namba za usajili T 227 CLA lililokuwa likitoka wilayani Ngara
mkoani Kagera kwenda wilayani Kahama mkoani
Shinyanga na Lori aina ya Fuso lenye namba za usajili T 621 ATD lililokuwa
limepakia matofali.
Taarifa
kutoka jeshi la polisi imesema kuwa chanzo cha ajali hiyo ni uzembe wa dereva
wa Hiace kwa kutokuwa mzoefu katika barabara ambaye alikuwa akiendesha gari kwa
mwendo kasi na kuingia katika makutano
ya barabara hiyo, bila kutazama magari mengine hali iliyosababisha gari lake
kugongwa na Lori hilo.
Majeruhi
wanane wa ajali hiyo wamelazwa katika hospitali ya Murgwanza huku miili ya
waliofariki ikiwa imehifadhiwa katika hospitali ya Nyamiaga wilayani Ngara
mkoani Kagera.
Source:Radio
Kwizera FM.
dah,Mungu azilaze roho za maheremu hao mahali pema na walojeruhiwa wapate nafuu mapema
ReplyDeleteMwenyezi Mungu azilaze Roho za Marehemu Mahala pema peponi.... Amen.
ReplyDeleteNi ajali ambayo inaumiza kwani kimefariki kichanga na mama yake mzazi aliyetoka kujifungua,kweli inauma na kuna taarifa wamefika 9 sasa waliokufa
ReplyDelete