![]() |
Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. |
Ligi Kuu msimu wa 2013/14 itaanza
Agosti 24 na itashirikisha timu 14.
Timu hizo ni mabingwa watetezi Yanga, Simba, Azam FC, Ashanti United,
Tanzania Prisons, Rhino Rangers na Kagera Sugar, Mtibwa Sugar, JKT Ruvu, Ruvu
Shooting, Mgambo Shooting, Mbeya City, JKT Oljoro na Coastal Union.
Vifuatavyo ni viwanja 10
vitakavyotumika kwa ajili ya mechi mbalimbali za Ligi Kuu msimu huu:
1.Uwanja
wa Taifa, Dar es Salaam.
Sifa za uwanja huu:
Uwanja huu ulianza kutumika mwaka
2007. Uwanja huu una vipimo vya mita 105 kwa meta 68 na una milango 35 kwa
ajili ya watazamaji kuingia na kutoka uwanjani. Una uwezo wa kuchukua zaidi ya
mashabiki 50,000.
Klabu zitakazoutumia uwanja huu
kama uwanja wake wa nyumbani ni Simba SC na Yanga SC.
2.Uwanja
wa Ali Hassani Mwinyi, Tabora.
Sifa za Uwanja huu:
Ulijengwa mwaka 1987 chini ya
usimamizi wa aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Lawrence Gama.
Una uwezo wa kuchukua watazamaji
30,000 na una milango minane kwa ajili ya kuingia na kutoka uwanjani.
Uwanja huu unamilikiwa na Chama cha
Mapinduzi (CCM).
Klabu itakayoutumia uwanja huu kama
uwanja wake wa nyumbani ni Rhino Rangers.
3.Sheikh
Amri Abeid, Arusha.
Uwanja huu ulijengwa mwaka 1957 na
unamilikiwa na Chama cha Mapinduzi (CCM).
Uwanja wa Sheikh Amri Abeid una
uwezo wa kuingiza watazamaji 25,000 kwa wakati mmoja.
Klabu ya JKT Oljoro inayomilikiwa
na Jeshi la Kujenga Taifa (JKT),
itautumia Uwanja wa Sheikh Amri Abeid kama uwanja wake wa nyumbani.
4.Uwanja
wa Sokoine, Mbeya.
Sifa za uwanja huu:
Unapatikana katikati ya jiji la
Mbeya na ulijengwa mwaka 1977. Uwanja wa Sokoine una uwezo wa kuchukua
watazamaji 20,000 na unamilikiwa na Chama cha Mapinduzi (CCM).
Klabu za Tanzania Prisons na Mbeya
City zitautumia uwanja huu kama uwanja wao wa nyumbani.
5.
Azam Complex- Chamazi, Dar es Salaam.
![]() |
Azam Complex- Dar es Salaam. |
Sifa uwanja huu:
Ujenzi wake ulianza mwaka 2010
chini ya mkandarasi Kampuni ya Salehe Msahala Contractors Limited.
Uwanja wa Azam Complex una vipimo
vya mita 110 kwa mita 71, pia una milango minne na una uwezo wa kuingiza
watazamaji 7, 000 kwa mara moja.
Klabu zitakazoutumia uwanja huu
kama uwanja wake wa nyumbani ni Ashanti
United, Azam FC na Ruvu Shooting.
Mmiliki wa uwanja huu ni klabu ya Azam FC.
6.
Uwanja wa Mabatini, Pwani.
Uwanja wa Mabatini unapatikana
katika mji wa Mlandizi uliopo Wilaya ya Kibaha mkoani Pwani. Ni uwanja
unaomilikiwa na Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) kambi ya Ruvu.
Klabu ya Ruvu Shooting itautumia
uwanja huu kwa ajili ya mechi zake za nyumbani isipokuwa zile itakazocheza
dhidi ya Simba SC na Yanga SC.
7.Uwanja
wa Kaitaba-Bukoba, Kagera.
Sifa za uwanja huu:
Una vipimo vya ukubwa wa mita 110
kwa mita 50. Ulijengwa mwaka 1957 na unamilikiwa na Manispaa ya mji wa Bukoba.
Uwanja wa Kaitaba
Una milango minne na una uwezo wa
kubeba watazamaji 5, 000 kwa wakati mmoja.
Klabu ya Kagera Sugar ndiyo
itakayoutumia uwanja huu kama uwanja wake wa nyumbani.
8.Uwanja
wa Mkwakwani, Tanga.
Sifa za uwanja huu:
Ulijengwa mwaka 1975 na Kampuni ya
Amboni Plantation. Uwanja wa Mkwakwani una vipimo vya ukubwa wa mita 105 kwa
mita 68, pia una milango saba na uwezo wa kuchukua watazamaji 20,000.
Mmiliki wa uwanja huu ni Chama cha
Mapinduzi (CCM).
Klabu za Coastal Union na Mgambo
Shooting zitautumia uwanja huu kama uwanja wao wa nyumbani.
9.Uwanja
wa Manungu, Morogoro.
Sifa za uwanja huu:
Ulijengwa mwaka 1988 ukiwa na
vipimo vya ukubwa wa mita 100 kwa 75. Uwanja
wa Manungu una milango minne na uwezo wa kubeba watazamaji 8,000.
Mmiliki wa uwanja huu ni Kampuni ya
Mtibwa Sugar. Klabu ya Mtibwa itautumia uwanja huu kama uwanja wa nyumbani,
lakini itakapokabiriana na Simba SC au Yanga SC itatumia uwanja wa Jamhuri Morogoro.
Uwanja wa Jamhuri, Morogoro
ulijengwa mwaka 1978 na unamilikiwa na
CCM na una uwezo wa kuchukua watazamaji 20,000.
LIGI KUU VODACOM 2013/2014 :-RATIBA YA MECHI ZA UFUNGUZI:
Jumamosi Agosti 24,2013.
YANGA |
v |
ASHANTI UNITED |
UWANJA WA TAIFA |
DSM |
MTIBWA SUGAR |
v |
AZAM FC |
MANUNGU |
MOROGORO |
JKT OLJORO |
v |
COASTAL UNION |
SH. AMRI ABEID |
ARUSHA |
MGAMBO JKT |
v |
JKT RUVU |
MKWAKWANI |
TANGA |
RHINO RANGERS |
v |
SIMBA |
A.H. MWINYI |
TABORA |
MBEYA CITY |
v |
KAGERA SUGAR |
SOKOINE |
MBEYA |
RUVU SHOOTINGS |
v |
PRISONS |
MABATINI |
PWANI |
No comments:
Post a Comment