Wanafunzi wa
kiume shule ya msingi Rulenge wilayani Ngara wakiwa katika foleni ya kupata
huduma ya choo katika matundu yenye milango.
|
Wanafunzi wa
shule ya msingi Rulenge wilayani Ngara wakiwa katika foleni ya kufanya usafi wa
vyoo vilivyojaa huku wanafunzi wenzao wakisaidia ovyo na kuharibu mazingira.
|
Vyoo vya
shule ya msingi Rulenge vikiwa baadhi yake havina hata milango na wanafunzi
kuogopa kuvitumia wakihisi kupata magonjwa ya mlipuko.
|
Na Shaaban
Ndyamukama.
Idara ya elimu katika Halmashauri ya
wilaya ya Ngara mkoani Kagera imeweka mpango mkakati wa kufaulisha wanafunzi wa darasa la saba kwa
asilimia 90 katika mitihani ya kuhitimu elimu ya msingi inayotarajia kuanza
Septemba 11 na 12 mwaka huu.
Hayo
yamebainishwa na Afisa elimu wilayani
Ngara Bw Simon Mumbee wakati akiongea na Mwandishi wa Habari hizi ofisini kwake kuhusu utekelezaji
wa maazimio ya Big Results Now
iliyowekwa na waziri wa elimu na mafunzo ya ufundi Dr.
Shukuru Kawambwa hivi karibuni jijini Dares Salaam.
Bw Mumbee
alisema kiwango cha asilimia hizo ni kutoka asilimia 70 katika miaka minne
iliyopita kwani changamoto kubwa ya
vitendea kazi hasa vitabu kwa
walimu na wanafunzi imepungua baada ya serikali kutoa vifaa hivyo.
Aidha alisema katika kutekeleza maazimio hayo walimu
na wanafunzi watakaokuwa katika ufaulu mzuri watapata motisha mbali mbali ili
kuwajengea uwezo wa kujituma katika kutekeleza na kutimiza majukumu yao.
“Haya ni
malengo ya wilaya na mkoa mzima wa kagera na jambo muhimu ni kuhakikisha walimu
wanafundisha kwa kuzingatia mihtasari ya masomo kwa kuwa na maandalio ya kila
siku na maazimio ya kazi huku wakiingia darasani kufundisha”.Alisema Mumbee.
Wakati
mikakati hiyo ikiwekwa na idara hiyo,Uhunguzi wa Mwanawamakonda Blog, imebaini wanafunzi wa shule
ya msingi Rulenge mjini wilayani Ngara wanaosoma darasa la kwanza na la pili wakijifunza kwa
kukalia vigoda kwa kukosa madawati.
Mwalimu mkuu
wa shule hiyo Mashaka makemba amesema kuwa shule hiyo ina jumla ya wanafunzi
1374 na serikali ya kijiji ilikuwa na mpango wa kujenga shule mpya
Alisema kuwa
changamoto nyingine ni wanafunzi wa shule hiyo kukosa huduma ya vyoo kwani
vilivyopo vimejaa huku wanafunzi wa elimu ya awali hadi darasa la tatu wakijisaidia
ovyo na kuchafua mazingira.
Hata hivyo
alisema juhudi za kujenga shule mpya ili kupata vyumba vya madarasa pamoja na
matundu ya vyoo zimegonga mwamba baada ya ardhi iliyolengwa kuwekwa shule kuwa na mgogoro kati ya serikali ya kijiji na Mwenyekiti
mstaafu wa CCM mkoani Kagera Pius Ngeze anayedai kuwa na hati miliki ya eneo
hilo.
No comments:
Post a Comment